Monday, January 14, 2013

mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya bia ya serengeti steve gannon atembelea mjengoni clouds media group.



Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group,Joseph Kusaga 'Joe' pichani kushoto akichanganua jambo kwa Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon mara baada ya kutembezwa studio mpya na ya kisasa kabisa,iliyofungwa mjengoni humo,ambayo inatarajia kuanza kutumika hivi karibuni,Steve Gannon amefanya ziara fupi mwishoni mwa wiki na kutembelea vitengo vyote kampuni hiyo huku akijionea namna shughuli mbalimbali zinavyofanyika mjengoni humo.
Steve Gannon akitazama picha za wasanii mbalimbali wa nje waliowahi kufika nchini Tanzania na kufanya maonesho yao kadhaa ndani ya ofisi za Prime Time Promotions Ltd.

Mkurugenzi wa mambo ya utafiti na vipindi vya Clouds Media Group,Ruge Mutahaba akifafanua jambo kwa Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon ambaye nae alikuwa akimsikiliza kwa makini.
Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon akimuuliza jambo mtangazaji wa kipindi cha Power Breakfast,Gerald Hando kuhusiana na mambo mbalimbali ya kikazi,alipotembezwa kwenye studio ya ziada.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group,Joseph Kusaga 'Joe' pichani kushoto akifafanua jambo kwa Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon mara baada ya kufanya ziara fupi mwishoni mwa wiki na kutembelea vitengo vyote kampuni hiyo huku akijionea namna shughuli mbalimbali zikifanya mjengoni humo.

Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon akizungumza jambo na baadhi ya wafanyakazi wa kitengo muhimu cha kampuni hiyo cha Masoko.
Steve Gannon akisalimiana na Oparesheni Meneja wa Prime Time Promotions Ltd.Balozi Kindamba,mara alipotembelea ndani ya kampuni hiyo ambayo imekuwa ikijihusisha na matamasha mbalimbali likiwemo tamasha kubwa la Fiesta ambalo hufanyika kila mwaka.
Steve Gannon akisalimiana na Gerald Hando
Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon akioneshwa matoleo mbalimbali ya jariba la burudani la KITANGOMA linachapishwa na kampuni ya Prime Time Promotions.

Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon akipeana mkono na Mmoja wa wafanyakazi wa Prime Time Promotions,Godliva Nicholaus mara alipowasili ndani ya ofisi za kampuni hiyo.
Mkurugenzi wa mambo ya Masoko na Mauzo,Shebba Kusaga akifafanua jambo kwa Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon.
Chief Editor wa Clouds TV,Bwa.Kanyopa akitoa maelezo mafupi kuhusiana na ufanyaji wao kazi ikiwemo na urushaji wa vipi kupitia Tv yao,Pichani kushoto ni Boss Joe akisikiliza kwa makini.


Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon alitembezwa pia ndani ya chumba maalum cha kuandalia habari,hapa Mtangazaji wa kipindi cha Michezo Shaffih Dauda akifafanua jambo kwa Steve Gannon.
Baada ya ziara kutembelea vitengo mbalimbali vya kampuni hiyo,pia Steve Gannon alipata wasaa wa kukaa meza moja na uongozi wa juu wa kampuni hiyo na kuzungumza machache,ikiwa ni sehemu ya mchakato wa ufanisi wa kikazi kwa mwaka mpya wa 2013. 
 
 
 
 

BALOZI WA NIGERIA NCHINI MAREKANI AMFANYIA DINNER YA KUMUAGA BALOZI WETU MH. MWANAID MAAJAR


Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Mwanaidi Maajar (wapili toka kulia)akiingia nyumbani kwa Balozi wa Nigeria (hayupo pichani) Potomac, Maryland, huku wakipokelewa na afisa ubalozi wa Nigeria (wa kwanza kulia) anayesalimia ni mama Lily Munanka ambaye ni mkuu wa utawala na fedha Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani akifuatiwa na mume wa Balozi, Bwn. Shariff Maajar siku ya Jumapili January 6, 2013 siku Balozi wa Nigeria alipomfanyia chakula cha jioni maalum kwa ajili ya kumuaga Balozi wetu ambaye anamaliza muda wake.
Mhe. Mwanaidi Maajar akilakiwa na Balozi wa Nigeria nchini Marekani, Mhe.Adebowale Ibidpo Adefuye siku ya Jumapili January 6, 2013 alipomkaribisha chakula cha jioni maalum kwa ajili ya kumuaga Balozi wa Tanzania nchini Marekani ambaye anamaliza muda wake.
Mke wa Balozi wa Nigeria akisalimiana na kumkaribisha Mhe. Mwanaidi Maajar huku mumewe Bwn. Shariff Maajar akiwa amesimama kwenye ngazi akiangalia.
Balozi na mumewe Bwn. Shariff Maajar wakisalimiana na Rais wa Jumuiya ya Watanzania DMV, Bwn Idd Sandaly ambaye pia aliongozana na mkewe (wakwanza kushoto) kwenye chakula cha jioni alichoandaliwa Balozi wetu na Balozi wa Nigeria kwa ajili ya kumuaga siku ya Jumapili January 6, 2013 nyumbani kwake Potomac, Maryland.
Kutoka kushoo ni Rais wa Jumuiya ya Watanzania DMV akiwa pamoja na mkewe, Balozi wa Benin nchini Marekani Mhe.Cyrille S. Oguin katika picha ya pamoja na Balozi wa Nigeria nchini Marekani Mhe.Adebowale Ibidpo Adefuye.
Balozi wa Nigeria nchini Marekani Mhe.Adebowale Ibidpo Adefuye (kulia) akisalimiana na Mume wa Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Bwn. Shariff Maajar.
Balozi wa Nigeria nchini Marekani Mhe.Adebowale Ibidpo Adefuye akisalimiana na kumkaribisha Balozi wa Botswana nchini Marekani Mhe. Tebelelo Seretse nyumbani kwake Potomac, Maryland siku ya Jumapili January 6, 2013 alipomualika chakula cha jioni maalum kwa ajili ya kumuaga Balozi wetu ambaye anamaliza muda wake.
Balozi wa Botswana nchini Marekani Mhe. Tebelelo Seretse (kushoto) akiongea jambo na Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Mwanaidi Maajar.
Kutoka kushoto ni Mkuu wa Utawala na Fedha Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, mama Lily Munanka, Mke wa Balozi wa Zimbabwe, Balozi wa Zimbabwe nchini Marekani, Mhe. Dr. Machivenyika Mapuranga na Balozi wa Benin nchini Marekani Mhe. Cyrille S. Oguin.
Wakati wa chakula.Picha na Vijimambo Blog
 

No comments:

Post a Comment