Monday, October 22, 2012

Mary Chizi aibuka kidedea kwenye Mashindano ya Michezo kwa Warembo wa Redd's Miss Tanzania 2012 jijini Dar

 
Mshiriki wa Redd's Miss Tanzania 2012,Mary Chizi ndie alieibuka kidedea leo katika mashindano ya Michezo mbali mbali iliyowashirikisha warembo wote wa Redd's Miss Tanzania 2012,ambapo yeye ameweza kuwa kinara katika michezo mitatu mfululizo ukiwemo wa kuogelea na kuwaacha wenzake wakijikongoja.Mary Chizi anaungana na wenzake wawili walioshinda mataji ya Miss Photogenic (Lucy Stephan) na Top Model (Magdalena Roy) ambao kwa pamoja wataingia moja kwa moja katika hatua ya nusu fainali ya Redd's Miss Tanzania 2012 mwaka huu.
 Warembo walioingia hatua ya Tano Bora katika mashindano ya Michezo Mbali mbali wakiwa kwenye picha ya pamoja.
 Warembo wa tatu waliojihakikishia kuingia hatua ya nusu fainali ya Mashindano ya Redd's Miss Tanzania 2012.Kutoka kulia ni Lucy Stephan (Redd's Miss Photogenic),Mary Chizi (Redd's Miss Tanzania Sports Lady) pamoja na Magdalena Roy (Redd's Miss Tanzania Top Model).
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino Agency ambao ndio waandaaji Mashindani ya Miss Tanzania,Hashim Lundenga akitangaza mshindi wa jumla kwenye Michezo mbali mbali.
 Bw. Yasson Mashaka akitangaza washindi wa Michezo yote kabla ya kutangaza warembo walioingia hatua ya tano bora.
 Warembo wa Redd's Miss Tanzania wakitoana jasho kwenye michezo mbalimbali hii leo Warembo wa Redds Miss Tz wakishiriki kwenye mchezo wa wavu hii leo kwenye fukwe ya bahari ya hindi kwenye mwendelezo wa maandalizi ya fainali ya Redds Miss Tz hapo mwezi ujao. mbio za Magunia.
Mchezo wa Soka.
 Mkuu wa Itifaki wa Kamati ya Miss Tanzania,Albert Makoye akitoa maelekezo wa warembo wa Redd's Miss Tanzania wakati wa kushindana kuruka umbali mrefu.
 Mchezo wa kuruka.
 Mpira wa Wavu.
 Kuvuta kamba.

RAIS KIKWETE AKUTANA NA UJUMBE KUTOKA KENYA LEO IKULU DAR ES SALAAM



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa  Jakaya Mrisho Kikwete ametaka wananchi wa Kenya wapewe nafasi ya kuamua ni viongozi gani wanawataka katika Uchaguzi Mkuu uliopangwa kufanyika Machi mwakani.
Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa wananchi wa Kenya wanayo haki ya msingi kabisa kuamua hatma ya taifa lao katika Uchaguzi Mkuu huo.
Mheshimiwa Rais aliyasema hayo leo Oktoba 21, 2012 alipokutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa wabunge wa vyama mbalimbali vya siasa vya nchini Kenya uliomtembelea Ikulu jijini Dar es salaam.
Ujumbe huo uliongozwa na Naibu Waziri Mkuu wa Kenya na Waziri wa Fedha Mhe. Uhuru Kenyatta ambaye pia ni Mwenyekiti wa  chama cha TNA na Waziri wa Sheria wa Kenya Mhe Eugene Wamalwa wa chama cha New Ford Kenya. Wote wawili ni wagombea wa nafasi ya Urais katika uchaguzi ujao.
Wengine katika msafara huo walikuwa ni Naibu Waziri wa Afya na mbunge wa Mombasa Mhe. Kambi Kazungu, Mbunge wa kuteuliwa wa chama cha TNA  Bi Rachel Shebesh, na Mbunge wa Kajiado kwa tiketi ya TNA Moses ole Sakuda na mbunge wa zamani Mhe Abdullahi Alli.
Rais Kikwete aliwapongeza kwa kuamua kufanya kazi kwa pamoja licha ya kuwa watakuwa  washindani katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu huo.
Mheshimiwa Rais ameitakia heri nchi ya Kenya katika uchaguzi huo ujao, na kusisitiza kwamba nchi hiyo ya jirani ina umuhimu katika mustakabali wa kiuchumi kwa nchi  za Afrika Mashariki.
Rais Kikwete wakati huo akiwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) alikuwa miongoni mwa viongozi walioshughulika sana kutafuta ufumbuzi wa ghasia na vurugu zilizozuka kufuatia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2007 nchini Kenya.
Rais Kikwete alikaa siku tatu nchini Kenya akitafuta usuluhishi wa vurugu hiyo ya kisiasa nchini humo, ambayo katika mazungumzo yake leo ameyataja kama ajali iliyolipata Taifa la Kenya, na ambayo majirani wake hawaitarajii kutokea katika uchaguzi ujao.
Mwisho
Imetolewa na:
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS
DAR ES SALAAM,
21 Oktoba, 2012
 

Tigo, American Garden wa-surprise watoto katika ‘Happy Birthday’ ya Andrew Chale

 Andrew Chale akiwa katika Picha ya Pamoja na Watoto ambapo walipewa zawadi mbalimbali na Kampuni ya Simu Za Mikononi ya TIGO
 Hii ndio Keki Iliyokatwa na Mdau Andrew Chale aliyesherehekea kumbukumbu ya kuzaliwa kwake na watoto waishio kwenye mazingira magumu
 Mdau Andrew Chale akikata keki tayari kwa kugawa kwa watoto waliohudhuria katika hafla fupi hiyo
Mtoto Mashaka Juma wa kituo cha Mitindo House, akimlisha keki kwa niaba ya watoto wenzake zaidi ya 50 waliojitokeza wakati wa sherehe ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa mwandishi wa gazeti hili Andrew Chale,  jana iliyofanyika ndani ya viunga vya Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni jijini Dar es Salaam na kudhaminiwa na kampuni ya Tigo Tanzania na American Garden.
 Watoto wakishangilia na kufurahia pamoja  na Mdau Andrew Chale
Wenceslaus Kisarika ambae ni Marketing Manager wa K&K pamoja  Cons  Ltd, akifungua shampeni 
KAMPUNI ya Tigo Tanzania leo Oktoba 21, imeweza kufanya ‘surprise’ mbalimbali kwa watoto waliojitokeza katika siku maalum ya kuzaliwa kwa mdau na mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima na blog, Andrew Chale, iliyofanyika ndani ya viunga vya Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni jijini Dar es Salaam.
Katika party hiyo maalum, Andrew Chale amesema ni ya kwanza kabisa kwa Mtanzania kufanya hivyo kwani ilianza tokea           Oktoba Mosi  kwa kutembelea vituo vya watoto waishio kwenye mazingira magumu na hatarishi  na kutoa misaada na pia kutembelea watoto mahospitalinio na kuwafariji.
Akielezea mtandao huu, Andrew Chale anasema alimwamini Mungu muda wote ndio maana ameweza kufika hapo na pia kutumia nafasi hiyo kwa pamoja kufurahi na watoto hao wakiwemo wale waishio kwenye mazingira magumu.
“Leo, ni siku muhimu sana kwangu, najiona nipo na mamilioni ya marafiki kwa kufika kwenu kumenitia sana faraja Mungu awabariki nyote” alisema Andrew  wakati akiwashukuru watoto mbalimbali waliojitokeza kufanya nao sherehe hiyo.
Watoto hao wakiwemo waliotoka kwenye vituo vya kulelea watoto vikiwemo vya  Tanzania Mitindo House kilicho chini ya Mbunifu,Khadija Mwanamboka, New Life Orphanage center  cha Kigogo, watoto waishio mitahani na wale wa majumbani walijumuika kwa pamoja na kufurahia na ‘Uncle’ wao Andrew Chale  ikiwemo kutembelea sehemu kadhaa za ndani ya jumba hilo la kumbukumbu na kujionea mambo mbalimbali.
Furaha hiyo ya siku maalum ya kuzaliwa kwa Andrew Chale imeweza kuongezwa utamu na kampuni ya Mawasiliano ya mtandao wa simu nchin, Tigo Tanzania, ambayo iliwezesha kumpatia keki na shampeni  maalum pamoja na zawadi zingine nyingi kwa watoto.
Kwa upande wake Ofisa wa masoko wa tigo, Benny  Lutaba, alipongeza kwa sherehe hiyo na kuomba jamii kuendelea kuwaunga mkono kwa bidhaa zao hapa nchini sambamba na kusaidia jamii kwa rika zote.
Nae Wenceslaus Kisarika ambae ni Marketing Manager wa K&K pamoja  Cons  Ltd  alipongeza kwa hatua ya watu kukumbuka watoto hasa waishio kwenye mazingira hatarishi na magumu hapa nchini.
“Tumefarijika sana kuunga kwenye siku hii muhimu, hakika jamii iiige mfano huu wa kuwakumbuka watoto hasa wanaohitaji msaada si utoe fedha hata kuwaleta mahala kama hapa ni moja ya kuwatimizia mahitaji yao” alisema Wence.
Aidham mbali na tigo,  American Garden kwa upande wao waliweza kuwa ‘surprise’ watoto  kwa kuwapatia zawadi za bidhaa zao zinazopatikana nchini kote.
 
Akizungumza na mtandao huu kwenye sherehe hiyo, Ofisa masoko wa Kingsway International (T) ltd,  American Garden, Miraji Chambuso  alipongeza kwa hatua hiyo ya kuwakumbuka watoto hao na ni moja ya kuhamasisha utalii wa ndani.
“Watoto wanapopata nafasi ya kufika sehemu kama hizi ni kuhasisha utalii wa ndani na sisi tupo mstari wa mbele katika kuhakikisha watoto wanatimiza ndoto na malengo yao” alisema Miraji. 
 

Makamu wa Rais Dkt . Bilal kufungua Mkutano wa saba wa Kimataifa wa Wafanyabaishara wanawake jijini Dar es salaam kesho

Mwenyekiti wa Tanzania Women Chamber of Commerce (TWCC) Fatma Riyami (kulia) akiongea na waandishi  wa habari (leo) jijini Dar es salam juu ya Mkutano wa Saba wa Kimataifa wa Wanawake wafanyabiashara wa Nchi ya Mashariki mwa Afrika unaofanyika Tanzania kwa mara ya kwanza na unaotarajiwa kufunguliwa na Makamu wa Rais wa Tanzania Dr. Mohamed Gharib Bilal  . Kushoto ni Makamu wa Mwenyekiti wa TWCC Anna Matinde. Mkutano huo unafunguliwa tarehe 22.10.2012 katika Hotel Kunduchi Beach.
…………………………………………………………….
Na Tiganya Vincent-MAELEZO-Dar es salaam
Makamu wa Rais wa Tanzania Dkt. Mohamed Gharib Bilal anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi katika ufunguzi wa Mkutano wa Saba wa Kimataifa wa Wanawake wafanyabiashara wa Nchi ya Mashariki mwa Afrika unaonza kesho  jijini Dar es salaam kwa lengo la kuimarisha mtandao wao.
 Kauli hiyo imetolewa leo na Mwenyekiti wa Tanzania Women Chamber of Commerce (TWCC) Fatma Riyami wakati  akiongea na waandishi  wa habari  Ofisi kwake.
Amesema kuwa Mkutano huo ambao ni wa saba(7) unafanyika nchini Tanzania kwa mara ya kwanza tangu walipoanzisha ushirikiano huo wa wanawake wafanyabiashara kwa nchi za  Afrika Mashariki.
Mwenyekiti huyo amesema kuwa wajumbe wa Mkutano huo wanatarajiwa kutoka katika Nchi za Kenya, Uganda, Rwanda , Burundi, Ethiopia , Sudan Kusini na mwenyeji Tanzania.
Amesema kuwa  Mkutano huo utakuwa fursa nzuri kwa wajumbe kutoka nchi zote saba kubadilishana uzoefu katika kazi ya kuwainua kiuchumi wakimama na kuimarisha Mtandao wa Wafanyabiashara wanawake katika Nchi za Afrika Mashariki.
 Ameongeza kuwa hatua hiyo itasaidia kufanya soko la wafanyabiasha wanawake wa Afrika Mashariki kuwa kubwa na hivyo kuwainua kiuchumi wakimama.
 Aidha Bibi Fatma Riyami amesema kuwa TWCC imeanzisha matawi katika Mikoa ya Kagera, Mwanza, Pwani, Dodoma, Mbeya, Dar es salaam na Arusha ikiwa na lengo la kutaka kuwa karibu na wafanfanyabiashara wanawake kwa nia kuimarisha Umoja wao.
 Wakati huo Mwenyekiti huyo amewasisitiza wajumbe wa Mkutano huo kufika katika Hoteli hiyo ifikapo saa 1.30 Asubuhi , Mgeni rasmi atafungua mkutano huo saa 2.00 kamili
 
 

Matukio katika picha ziara ya Rais Kikwete Oman

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza wakti wa mkutano na Watanzania waishio Oman uliofanyika jijini Muscat  hivi karibuni.Kulia ni Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe na kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Oman, Bwana Ali Ahmed Saleh
Baadhi ya Wafanyabiashara kutoka Tanzania na wenzao wa Oman wakiwa katika picha ya pamoja na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete muda wakati wa mkutano wa pamoja kati ya wanyabiashara wan chi hizo mbili uliofanyika katika Hoteli ya Al Bustan Palace jijini Muscat hivi karibuni.
Baadhi ya Wafanyabiashara kutoka Tanzania na wenzao wa Oman wakiwa katika picha ya pamoja na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete muda wakati wa mkutano wa pamoja kati ya wanyabiashara wanchi hizo mbili uliofanyika katika Hoteli ya Al Bustan Palace jijini Muscat hivi karibuni.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na watanzania mbalimbali waliohudhuria katika mkutano huo
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na baadhi ya Watanzania waishio Oman katika mkutano uliofanyika jijini Muscat wiki iliyopita
Baadhi ya Watanzania waishio Oman wakiimsalimia kwa shauku Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete muda mfupi baada ya kuongea nao jijini Muscat wakati wa ziara yake iliyomalizika hivi karibuni.Picha na Freddy Maro
 
 
 
 

No comments:

Post a Comment