Monday, October 22, 2012

Kiongozi wa Jumuiya ya UAMSHO Shekh Farid Hadi Ahmed akishuka kwenye gari la Polisi kuelekea Mahakama ya Mwanakwerekwe kwenda kusomewa mashtaka yao yanayomkabili ikiwemo kusababisha fujo na uchochezi.
Mmoja kati ya Viongozi wa UAMSHO Shekh Azan Khalid Hamdan (43) akishuka kwenye gari la Polisi kuelekea Mahakamani Mwanakwerekwe kwenda kusomewa mashtaka yao.

Gari la Polisi la pili ambalo liliwachukuwa Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO ambao walishitakiwa kwa makosa ya kufanya fujo na uchochezi likiwa linasindikizwa na magari ya Polisi kuja Mahakama ya Wilaya ya Mwanakwerekwe.
Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia wakiwa wanaimarisha usalama katika eneo la Mahakama ya Wilaya Mwanakwerekwe ambapo Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO walipelekwa kwenda kusomewa mashitaka yao.
Gari la Polisi ambalo liliwachukuwa Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO ambao walishitakiwa kwa makosa ya kufanya fujo na uchochezi likiwa linawasili Mahakama ya Wilaya ya Mwanakwerekwe.
Baadhi ya Wananchi walioenda Mahakamani hapo kwenda kushuhudia kesi inayowakabili Viongozi wa Jumuiya ya UAMSHO ambao walikosa dhamana na kurudishwa Rumande.Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.


Wanafunzi Buguruni Viziwi na Balozi wa Airtel AY-waomba Watanzania kuchangia vifaa vya kufundishia.

 
Balozi wa Airtel  nchini Ambwene Yessaya (AY) (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa chekechea ya shule ya msingi Buguruni Viziwi walipotembelea shule hiyo mwishoni mwa wiki hii.Airtel kwa kushirikiana na BAMVITA wanaendesha mradi maalum utakaowezesha wanafunzi hao wenye uhitaji maalum kupata vifaa vya kujifunzia.
Meneja huduma za jamii wa Airtel Hawa Bayumi akiangalia ujuzi wa wanafunzi wa shule ya Buguruni viziwa alipotembelea shule hiyo mwishoni mwa wiki hii. wakati AIRTEL na Balozi wao msanii AY walipofanya ziara maalum ya kuhamasisha jamii kuchangia wanafunzi hao wa shule ya msingi Buguruni viziwi kupata vifaa vya kujifunzia kwa kushirikiana na BAMVITA.
Mwalimu wa shule ya msingi Buguruni Viziwi akiwapa ujumbe wanafunzi wa shule hiyo baada ya kutembelewa na wafanyakazi wa Airtel, kutoka kushoto ni mwamlimu mkuu wa shule hiyo bi Winfrid Jeromia, akifuatiwa na Meneja huduma za jamii wa Airtel Hawa Bayumi na Airtel Ambassador Ambwene Yessaya (AY). Airtel kwa kushirikiana na BAMVITA wanaendesha mradi maalum utakaowezesha wanafunzi hao wenye uhitaji maalum kupata vifaa vya kujifunzia
Meneja huduma za jamii wa Airtel Hawa Bayumi akiongea na wanafunzi wa shule ya Buguruni Viziwi mwishoni mwa wiki hii wakati ambapo airtel walitembelea shule ya msingi viziwi kuhamasisha upatikanaji wa vifaa vya kufundishia pamoja na nyenzo mbalimbali kupitia mradi maalumu wa kuchangia vitabu unaoendeshwa na Airtel kwa kushirikiana na BAMVITA, kushoto ni Mwalimu wa shule hiyo bi Judith Kaneno akifuatiwa na Airtel Ambassador ajulikanae kwa jina la AY( Ambwene Yessaya) kulia ni Mwalimu mkuu bi. Winfrid Jeromia.


==========  =========  ==========

Wanafunzi Buguruni Viziwi na Balozi wa Airtel AY-waomba Watanzania kuchangia vifaa vya kufundishia.

Ni moja kati ya shule zitakazofaidika na mradi wa Airtel na BAMVITA

Wanafunzi wa shule ya Buruguni viziwi  wameomba watanzania na wadau mbalimbali kuchangia ili kufanikisha upatikanaji wa vifaa vya kufundishia pamoja na nyenzo mbalimbali kupitia mradi maalumu wa kuchangia vitabu unaoendeshwa na Airtel kwa kushirikiana na BAMVITA. Wanafunzi hao waliosema hayo wakati Airtel pamoja na balozi wake AY walipotembelea shuleni hapo mwisho mwa wiki hii.

Wanafunzi wa shule ya buruguni viziwi ambao mbali na masomo ya darasani pia wanafundishwa kazi za stadi, walionekana kufanya kazi za stadi za mikono ikiwemo kutengeneza shanga pamoja na mazulia madogo ya miguu, wametia hamasa na kuthibithisha kwamba  wakiwezeshwa na kupatiwa nyenzo wanauwezo mkubwa sana wa kufanya shughuli za stadi na ubunifu.

Akiongea katika ziara hiyo Meneja huduma za jamii wa Airtel Hawa Bayumi alisema “leo tumetembelea shuleni hapa ikiwa ni mwendelezo wa utaratibu wetu katika kubainisha mahitaji ya ziada ambazo shule hizi zenye mahitaji maalumu zinahitaji. Shule ya Buruguni viziwi ni moja kati ya shule zitakazofaidika Mradi huu unaoshirikisha Airtel na BAMVITA una lengo la kusaidia kuendeleza kiwango cha Elimu hapa nchini na kutoa nafasi kwa jamii yetu kuweza kushiriki na kuchangi elimu ya msingi kwa watoto wenye mahitaji maalum. ‘

Naye Balozi wa Airtel AY Ambwene Yesaya alisema “ Tunawashukuru watanzania kwa kuitikia wito na kuanza kuchanga na tunaendelea kutoa wito kwa watanzania kuendelea kuchangia kwa kutuma neno “Vitabu” kwenda namba 15626 na kwakufanya hivyo kila SMS utakayotuma utakuwa umechangia shilingi 200 au kuchangi kiwango chochote kupitia Airtel money 0788 041361 ambapo jina la fumbo ni VITABU.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Buguruni Viziwi bi. Winfrid Jeromia alikuwa na haya ya kusema”tunaishukuru sana Airtel kwa kuweza kuja na mradi kama huu wa kuweza kuinua Elimu hapa nchini na kurahisha mazingira yetu ya ufundishaji hapa shuleni. Tunawaomba watanzania wengine na makampuni mengine makubwa yajitokeze kwa wingi kuweza kuchangia katika mradi huu ili kuinua wigo wa Elimu hapa nchini.

Kampeni hii ya kuchangia vifaa kwa shule zenye mahitaji maalumu inayoendeshwa na Airtel kwa kushirikiana ilizinduliwa Agosti 23 2012 na itaendelea kwa muda kwa mienzi mitatu. Kwa kuanzia shule tatu za jijini Dar es Salaam ambazo ni Uhuru Mchanganyiko, Sinza Maalum, na Buguruni Viziwi zitafaidiaka na mradi huu.
 

Kivuko cha Mto Kilombero

Kivuko cha Mv Kilombero Na. 1 kikivusha wananchi na mali zao juzi Mto Kilombero, mkoani Morogoro kufuatia kivuko cha awali cha Mv Kilombero Na. 2 kuleta hitilafu katika mfumo wa usukani. Picha na  Juma Mtanda
 
 

Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad:'CUF itaendelea kuwaunganisha Watanzania.'

 Wafuasi na wapenzi wa CUF wakimsikiliza Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar na Katibu Mkuu wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad wakati akiwahutubia katika viwanja vya Buguruni jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad akiwahutubia wafuasi ya wapenzi wa chama hicho katika viwanja vya Buguruni jijini Dar es Salaam.
  Aliyekuwa Mkurugenzi wa ulinzi na usalama wa ADC Bw. Al-Badawi akizungumza katika mkutano wa hadhara wa CUF baada ya kuamua kurejea CUF akitokea ADC. Kabla ya kwenda ADC na baadae kurejea CUF Al-Badawi alikuwa mwenyekiti wa CUF Wilaya ya Temeke
Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad akimkabidhi shati la chama hicho kijana Joseph Christian ambaye alikuwa katibu mwenezi wa CHADEMA tawi la Chuo Kikuu Dodoma. Joseph amekihama CHADEMA na kujiunga na CUF kwenye mkutano wa hadhara huko Buguruni jijini Dar es Salaam.Picha na Salmin Said-Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar 
---
Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar na Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad amesema chama chake kitaendelea kutetea na kutekeleza sera yake ya kuwaunganisha watanzania popote walipo bila ya ubaguzi wa aina yoyote.

Amesema operesheni mchakamchaka hadi mwaka 2015 iliyozinduliwa na chama hicho hivi karibuni imekuwa ni sehemu ya utekelezaji wa sera hiyo,na kwamba tayari imeanza kuleta mafanikio katika mikoa iliyoanza kutekelezwa ukiwemo mkoa wa Arusha.

Maalim Seif ametoa kauli hiyo katika viwanja vya Buguruni jijini Dar es Salaam alipokuwa akiwahutubia wafuasi na wapenzi wa chama hicho kwenye mkutano maalum wa hadhara uliolenga kuwakaribisha wanachama wapya na kuwapokea wanachama walioamua kurejea CUF baada ya kukihama na kuhamia vyama vyengine.Katika mkutano huo Maalim Seif aliwapokea na kuwapa kadi za chama hicho wanachama kadhaa walioamua kurejea chama hicho wakitokea chama cha ADC wakiongozwa na aliyekuwa Mkurugenzi wa ulinzi na usalama wa ADC Bw.Al-Badawi.
Kabla ya kujiunga na ADC, Bw. Al-Badawi alikuwa mwenyekiti wa CUF Wilaya ya Temeke, na sasa ameamua kurejea CUF kwa kile alichokieleza kuwa ni ubabaishaji ndani ya chama hicho kipya kinachohusishwa na mbunge wa jimbo la Wawi Mhe. Hamad Rashid Mohd.
 
Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar amesema Tanzania imekuwa ikipita katika kipindi kigumu cha migogoro na uvunjifu wa amani, mambo ambayo yanapaswa kupigwa vita ili kurejesha hali ya amani na kuvumiliana.

Amedai kuwa chanzo kikuu cha migogoro ya kijamii ikiwemo ya ardhi na mizozo ya kidini inatokana na kutokuwepo kwa mikakati imara ya kuendesha nchi, na kwamba viongozi wanapaswa kujifunza kutokana na migogoro hiyo, ili kuweka mikakati imara ya kuendesha nchi kwa uhakika. 
 
“Nchi haiendeshwi kwa kuigiza, bali kwa kuwa na viongozi wenye dira ya mabadiliko kwa maendeleo ya wananchi”, alisisitiza Maalim Seif.
 
Amesema kutokana na viongozi kutokuwa na dira na mikakati imara ya kuendesha nchi, Watanzania wameshindwa kunufaika na rasilimali za nchi yao ambazo ni nyingi na zinaweza kuwabadilisha kiuchumi.
Amefafanua kuwa iwapo wananchi watanufaika moja kwa moja na rasilimali zao, wataweza kuzitunza na kuzilinda ili ziwe endelevu, na kwamba kinyume chake ni kuzihujumu rasilimali ambazo watahisi haziwanufaishi.
 
“Popote pasipo na haki hakuna amani, tunataka kila Mtanzania ajihisi kuwa ana haki sawa katika nchi hii, sio kuwa na raia wa madaraja, yaani daraja la kwanza, la pili na latatu”,alifahamisha huku akishangaliwa na umati wa watu waliojitokeza kwenye mkutano huo.

Katika hatua nyengine, aliyekuwa katibu mwenezi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA katika tawi la Chuo Kikuu Dodoma bw. Joseph Christian amejiengua katika chama hicho na kujiunga na CUF.
 
Akizungumza katika mkutano huo bw. Joseph amesema ameamua kujiengua CHADEMA na kujiunga na CUF kwa madai kuwa chama hicho kimekuwa kikiendeshwa kwa misingi ya undugu na ukabila, na kuwatelekeza vijana wenye lengo la kuleta mabadiliko ya kisiasa nchini.

Amewatahadhamisha vijana kuwa makini na sera za chama hicho na kuacha kukurupuka kuvamia sera za vyama wasivyovifahamu.Nae Mwenyekiti wa ADC Wilaya ya Kinondoni Bw. Saburi Mtoro, ambaye pia ameamua kukihama chama hicho na kujiunga na CUF amemuahidi Katibu Mkuu wa CUF kuwa wanachama wote wa ADC katika Wilaya hiyo watajiunga na CUF.
 
 

MAKAMU WA RAIS DK GHARIB BILAL AKIHUTUBIA WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA AKINA MAMA WAJASIRIALIAMALI KUTOKA NCHI ZA UKANDA WA AFRIKA MASHARIKI.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa akina Mama Wajasiliamali kutoka Nchi za Ukanda wa Afrika, uliofanyika leo Oktoba 22, kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Kunduchi Beach jijini Dar es Salaam, ukiwa ni mkutano wa kwanza kufanyika nchini Tanzania.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungao wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano wa akina Mama Wajasiliamali kutoka Nchi za Ukanda wa Afrika, uliofanyika leo Oktoba 22, kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Kunduchi Beach jijini Dar es Salaam, ukiwa ni mkutano wa kwanza kufanyika nchini Tanzania. Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais
 

Ukumbi Walipuka kwa Shangwe Baada ya Rais Jakaya Kikwete Kuwasili na Kuhutubia Kwenye Kilele cha mkutano mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)Mjini Dodoma


Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili katika ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma kufunga mkutano mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)
Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiiimba na kucheza nyimbo mbalimbali katika ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma alipowasili leo kufunga mkutano mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)
Mwenyekiti wa UWT  Sophia Simba akiongea katika ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma baada ya kufunga mkutano mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)
 Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia katika ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma kufunga mkutano mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)
 Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mwenyekiti wa UWT  Sophia Simba na Katibu Mkuu Amina  Makilagi katika ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma baada ya kufunga mkutano mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)
Sehemu ya wajumbe wa mkutano mkuu wa UWT wakicheza segere
Sehemu ya wajumbe wa mkutano mkuu wa UWT
Wanachama wakongwe wa UWT na CCM wakishangilia
Sehemu ya wajumbe wa mkutano mkuu wa UWT wakirushwa na Sizya Mazongela wa kundi la Segere
Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na wakongwe wa UWT katika ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma  baada ya kufunga mkutano mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)
Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na wake wa viongozi katika ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma baada  kufunga mkutano mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)
  Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipozi na wanachama wakongwe wa UWT Ikulu ndogo Dodoma katika mchaplo aliowaandalia wajumbe wa Umoja huo baada ya kutoka katika  ukumbi wa Chuo cha Mipango mjini Dodoma kufunga mkutano mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT).Picha na IKULU
 
 

TCRA: TV ZENYE MIGONGO NA MATUMBO MAKUBWA PIA ZITAPOKEA MATANGAZO YA DIGITALI

 Na Mohammed Mhina, Zanzibar 
 Imeelezwa kuwa TV zote zikiwemo zile zenye migongo, matumbo na viuno virefu zote zina uwezo sawa wa kupokea matangazo ya digitali na Watanzania waepuke uvumi wa watu wachache wanaodai kuwa TV  za zamani hazitapokea zitafutwa mara Tanzania itakapoingia kwenye mfumo wa Digitali.
\
 Wito huo umetolewa na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano hapa nchini TCRA ambaye pia na Mratibu wa Ofisi za Kanda Bw. Victor Nkya, wakati wa mkutano wa Wataalamu wa Mawasiliano ya Habadi kwa njia ya digitali kutoka nchi za SADC unaojadili umuhimu wa mfumo wa Digitali.
 Bw. Nkya amesema kuwa wananchi hawana haja ya kuwa na hofu juu ya TV walizonazo zikiwemo zenye matumdo na migongo mikubwa kuwa hazitaweza kupokea matangazo ya televishen katika mfumo mpya wa digitali.
 Amesema kutokana na watu wengi kutumia televishen za Analojia, ni lazima kila mmoja wetu awe na kingamuzi na kazi ya Mamlaka ya mawasiliano ni kuwajengea wananchi matumaini na kuepuka kudanganywa.
 Kwa siku za hivi karibuni baada ya Tanzania kuridhia mabadiliko ya mfumo wa Digitali, wananchi wamekubwa na wasiwasi wakidhani kuwa huo ndio mwisho wa tv za zamani.
 Awali akifungua Mkutano huo wa siku tatu hapa mjini Zanzibar, Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Zanzibar Mh. Rashid Suleiman, amewataka wananchi kukabiliana na changamoto mbalimbali zitakazojitokeza wakati wa mabadiliko ya kutoka katika mfumo wa analojia na kuingia katika digitali.
 Amesema ni vema wananchi wakahama mapema kutoka katika mfumo huo wa zamani ili kuepuka usumbufu wakati yatakapotokea mabadiliko hayo kwani hakutakuwa na muda wa nyongeza kama Watanzania walivyozoea.
 Na kuna umuhimu wa wananchi pia kusikiliza maelekezo ya wataalamu badala ya kusikiliza propaganda za watu wasio na ujuzi juu ya teknolojia hiyo.
 ”Watanzania hawana haja ya kuogopa na badala yake wajiandae kujipatia vingamuzi na kinyume cha hivyo watashindwa kupata matangazo ya televishen kama wanavyotarajia.” Alisema Waziri. 
Amesema kila mabadiliko yana hasara na faida zake, lakini kwa mabadiliko ya kutoka katika mfumo wa analojia kwenda digitali, kuna faida kubwa na moja ya faida hizo ni kuwawezesha watu wote kupokea matangaza sawa na yenye ubora unaofanana na kwa wakati muafaka.Mkutano huo wa siku tatu unazishirikisha nchi zote za Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika SADC ikiwemo  Angola, Afrika ya Kusini, Malawi, Namibia, Botswana, Swazlland, Lesotho, Msumbiji na wenyeji Tasnzania.
 
 
 
 

No comments:

Post a Comment