Wednesday, June 13, 2012

Watoto waangukiwa na nyaya za Umeme na kuujeruhiwa vibaya.

IMG-20120613-WA002
Watoto watatu ambao hawajatambuliwa majina yao wakiwa wamelala nyuma ya Pickup kwa ajili ya kupelekwa Hospitali baada ya kujeruhiwa na nyaya za umeme.
IMG-20120613-WA001
Watoto watatu ambao walikuwa wakitembea pembezoni mwa barabara wameangukiwa na nyaya za umeme baada ya gari dogo aina ya Escudo kugonga nguzo asubuhi maeneo ya Mbagala Zakheem.
Watoto hawa watatu ambao walikuwa wakitembea pembeni wamejeruhiwa vibaya na kuunguzwa sehemu mbalimbali kwenye miili yao, ambapo wasamalia wema waliwasaidia na kuwapakia kwenye gari kukimbizwa Hospitali.
Majumba Sita wafunga barabara


 Wakazi wa Eneo la Ukonga Majumba Sita Wilaya ya Ilala jijini Dar es sal;aam wafunga barabara kuu ya Nyerere katika eneo hilo la majumba sita kushinikiza kuwekwa kwa matuta katika eneo hilo kufuatia kukuthiri kwa ajali za wakazi wa eneo hilo kugongwa wavukapo barabara hiyo.

Tukio hilo lilitokea leo majira ya saa za asubuhi na kudumu hadi saa nane mchana baada ya kijana mmoja kungongwa katika eneo hilo akijaribu kuvuka barabara hiyo na kufa papo hapo.

Wakiwa na mabango, mawe na matofali wakazi hao waname, wanawake, wazee kwa watoto walifurika katika barabara hiyo na kushinikiza kuja kwa mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kuwekwa kwa matuta.
 Wananchi wakiwa wamefurika kwa wingi barabarani na hata Jeshi la polisi lililopfika na kuwasihi waruhusu magari kupita waligoma na huko mitaani pia walizuia boda boda (pikipiki) kupita hadi matuta yawekwe.
 Magari yakiwa yamezuiwa eneo hilo karibu na Kambi ya Jeshi Kikosi cha Anga.
 Wananchi wakiwa upande wa pili wa barabara kutaka kujua hatma ya usalama wao.
Watu walikuwa ni wengi. Awali eneo lingine katikati ya Njia Panda segerea na Minazi Mirefu (Banana) wanafunzi wa shule ya Msingi Minazi Mirefu waliwahi kuandamana barabarani hapo kushinikiza kuwekwa kwa matuta baada ya wenzao kadhaa kugongwa na serikali ikaweka matuta hayo na hivi sasa hali ni shwari katika eneo hilo. 
 
 
 
 

Uhaba wa madawati bado ni changamoto shule za msingi Musoma

Wanafunzi wa shule ya Msingi Etaro wakiwa darasani wakimfuatilia mwalimu.wanafunzi wengi katika shule hii wanakaa chini kutokana na uhaba wa madawati.
Wanafunzi wakiendelea na masomo yao huku wengine wakitumia magoti yao kama sehemu za kuandikia huku wakiwa wamekaa chini.
Uhaba wa madawati katika shule za msingi na sekondari umeendelea kuumiza vichwa vya wapenda elimu pamoja na wazazi kwa ujumla nchini.
 
Upungufu wa madawati katika shule za msingi umeendelea kudidimiza kiwango cha elimu nchini huku ukichangia kuongezeka kwa utoro kwa kusababisha wanafunzi wengine kukata tamaa ya kusoma na mazingira ya shule kwa ujumla ambayo si rafiki kwao.

Matokeo ya wanafunzi kukaa chini husababisha wanafunzi kuandika wakiwa wameinama na wengine hata kulala kifudi fudi na wengine kuchuchumaa na hivyo kushindwa kuandika vizuri na pia kuchoka mapema.Hali hii kupelekea matokeo mabaya nyakati za mitihani hasa ya kitaifa.
Hali halisi ndiyo hii wilayani Musoma vijijini
Wanafunzi wengine wakiyageuza madawati mabovu angalau wapate sehemu ya kukaa
Wengine wanatumia viatu vyao kukalia, na wasio na viatu wanakaa kwenye vumbi.Picha Na Haki Elimu
 

No comments:

Post a Comment