Thursday, June 7, 2012

Taswira Mbalimbali Za Muendelezo Wa Operesheni Okoa Kusini inayofanywa na CHADEMA


 Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akihutubia maelfu ya wananchi Masasi mjini
Mbunge wa jimbo la Ubungo (CHADEMA) John Mnyika akipandisha bendera ya chama nje ya ofisi ya CHADEMA Kijiji cha Mkangaula
  Pichani ni Mwenyekiti Freeman Mbowe akikata utepe wa kufungua Ofisi ya CHADEMA Kijiji cha Mkangaula. Ilikuwa ni baada ya Katibu Mkuu, Dkt. Slaa kutoa hotuba ya ufunguzi na John Mnyika kupandisha bendera ya chama nje ya ofisi hiyo, ikiwa ni ishara ya kupiga hatua katika mapambano ya awamu ya pili.
 Mbunge wa Ubungo(CHADEMA)John Mnyika akitoa 'somo' kwa wanakijiji wa vijiji vya Kata ya Lumesule. Mapema Mbunge wa Ubungo(CHADEMA)John Mnyika alikaribishwa na kuzungumza na Katibu wa Tawi wa CUF, Bi. Zaituni. Wananchi walimwelewa vyema. Kadi zikauzwa vizuri. Akaacha uongozi wa muda wa tawi lenye wanachama wa 34. Katika Kijiji hicho cha Lumesule,
  Mwananchi mmoja kwa jina la Yasin Mohamed alihoji Ya Mbunge wa Ubungo(CHADEMA)John Mnyika (Kulia)ilikuwaje CHADEMA wakaachia Dkt. Slaa ashindwe urais, wakati alichaguliwa kwa kura nyingi na wananchi na wao wanajua alishinda uchaguzi huo wa mwaka 2010.

 John Mnyika akiwa katika vijiji vya Kata za Makukwe na Mkwedu, wilayani Newala. Kwa George Mkuchika ambako alikutana na kiashiria cha wazi kuhusu udhaifu wa Waziri Mkuchika (Mbunge wa Newala) katika kusimamia majukumu yake, baada ya wananchi katika Kijiji cha Tengulengu, Kata ya Mkwedu kumlalamikia kuwa Diwani wa Kata hiyo, Juma Dadi hajawahi kufungua ofisi yake zaidi ya mwaka mmoja sasa. Pamoja na kuwasilisha malalamiko yao kwa barua Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Newala na kwa Mbunge wao, Mkuchika, hakuna hatua zozote zilizochukuliwa.
 Unaweza kuona pia wanawake wakiitikia PEOPLES POWER, nao wakaipiga ya nguvu kweli kweli kuonesha umoja na mshikamano katika Falsafa ya Nguvu ya Umma ya CHADEMA, katika kudai uwajibikaji, kupigania haki, uhuru na mabadiliko ya kweli ya mfumo na utawala nchini.
 
 Sehemu ya Umati mkubwa wa wananchi kwenye mkutano huo
Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Slaa akizongwa na wananchi wa Kijiji cha Namahinga, Masasi aliokuwa akisalimiana nao.
 Opresheni Okoa Kusini katika picha, hapa ilikuwa Masasi Mjini. Waweza kuona katika baadhi ya picha watu walivyopanga mstari kupigania kadi.Picha na Habari na Kurugenzi ya Habari- CHADEMA
 
 

Tawi la CHADEMA Washington DC Nchini Marekani Lazidi Kuvuna Wanachama Wapya

  Linda Bezuidenhout (LB) furaha baada ya kuvua kamba kuvaa kwanda na kuchukua kadi  kuwa mwanachama kamili wa Chama Cha Demokrasia Chadema.
 Mwenyeketi wa tawi la Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC Mhe. Kalley Pandukizi, pamoja na katibu wake  Mhe. Libe Mwang'ombe akimkabidhi rasmi mwanacham mkareketwa  ambae ni mwana mitindo Linda  Bezuidenhout (LB) kati ya uwanachama wa chama cha  Demokrasia Chadema katika ofisi ya  tawi la Tawi la Chama Washington DC.
 Mwenyeketi wa  Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC Kalley Pandukizi akiwa na katibu wachama hicho,Ndugu Libe Mwang'ombe alipotoa kadi rasmi kwa Beautician maharufu na designer wa kitanzan Linda  Bezuidenhout (LB)
 Viongozi wa tawi la chadema Washington DC wakipata Champagne
Mwenyeketi wa tawi la Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC Mhe.  Kalley pamoja na katibu wake  Mhe. Libe Mwang'ombe wakipata picha ya pamoja na Linda  Bezuidenhout Atlanta, Georgia na wanachama wa tawi la chadema Washington DC. Katika miaka ya nyuma Linda aliwahi  kusponsor  matukio mbali mbali kwenye  miaka ya 1990 wengi wao wakimjua kwa Linda Express Nchini Tanzania ambae ambaye hivisasa anajishughulisha na  biashara ya nguo za kiume milanovita.com pamoja na  zakike ambazo anadesign mwenyewe kwa brand name ya Linda kutoka Atlanta, Georgia Nchini Marekani.Picha na Mdau Wa Swahilivilla
 

MILIONI 421.8 ZAPATIKANA KUCHANGIA MPANGO WA ELIMU KATA YA KIPAWA JIJINI DAR ES SALAAM

Mbunge wa Jimbo la Segerea, Dk. Makongoro Mahanga (kulia), Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (kushoto) na Mwenyeji wa harambee ya kuchangia mpango wa elimu wa Kata ya Kipawa, Diwani wa Kata  hiyo Bonah Kaluwa, wakimuongoza Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa ambaye alikuwa mgeni rasmi kuingia ukumbini Katika hafla iliyofanyika jana usiku ndani ya hoteli ya Kilimanjaro (Kempiski hotel) jijini Dar es Salaam .
Wadau mbalimbali wakiwa kwenye harambee hiyo
Diwani wa Kata ya Kipawa Bonah Kaluwa, akitoa neno la shukurani kabla ya kuanza kwa harambee hiyo.
Mgeni rasmi wa Hharambee hiyo akimpa mkono wa asante mwakilishi wa kampuni ya Home Shopping Centre Bi Madiha Al Harthy (kushoto),Salma baada ya kuchangia sh. milioni 22.
Mkurugenzi wa SONGAS Limited Bw;Christopher Ford(katikati),akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya dolla za kimarekani 10,000, mgeni rasmi wa harambee hiyo.kushoto meneja rasilimali Songas Bi Agatha Keenja.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Shinyanga, Hamisi Mgeja (katikati) akipongezwa na Mgeni rasmi wa harambe hiyo baada ya kuchangia sh. 500,000.
eya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (kushoto), akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh.milioni 10, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, aliyekuwa mgeni rasmi katika harambee ya kuchangia mpango wa elimu Kata ya Kipawa, iliyofanyika Dar es Salaam juzi. Fedha hizo zilitolewa na Manispaa hiyo ambapo zaidi ya sh. milioni 400 zilipatikana.(PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE)
 
Na Dotto Mwaibale

WAZIRI Mkuu wa zamani , Edward Lowassa, ameendeleza kuwa mstari wa mbele katika harakati zake za kuchangisha mamilioni ya fedha baada ya kuchangisha Sh.421,850,000 kwa ajili ya kuboresha Mfuko wa Elimu Kata ya Kipawa katika Manispaa ya Ilala Jijini Dar es Salaam.

Lowassa ambaye ni mbunge wa Monduli (CCM), aliendesha harambee hiyo juzi katika hafla iliyofanyika Hoteli ya Kempiski Jijini Dar es Salaam ambapo yeye mwenyewe alichangia Sh.milioni 10.

Katika harambee hiyo miongoni mwa makampuni yaliyochangia kiasi kikubwa ni  Lion Club Sh.milioni 70, Home Shipping Center Sh.milioni 22, African Barrick Gold Dola 10,000, Songas Dola 10,000, Maersk Sea Line ilichangia Sh.Miliono 90, na Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja alichangia milioni Sh.10.

Wengine waliochangia ni madiwani, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi, Chadema, taasisi za watu binafsi na mtu mmoja mmoja ambapo Radio Clauds walitoa muda wa hewani wa kutangaza mpango huo wenye thamani ya sh. milioni 12.

Akizungumza kabla ya kuendesha harambee ya kuchangisha, aliwataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri kuendelea kuwahamasisha wananchi kuwekeza katika kuchangia sekta ya elimu.

Lowassa alimpongea Diwani wa Kata ya Kipawa, Bonnah Kaluwa, kwa jitihada zake alizozionyesha za kuchangia elimu na kuwataka madiwani wengine kuiga mfano huo.

Diwani wa Kata ya Kipawa,  Bonnah Kaluwa, kwaupande wake alisema shule saba za Msingi na Sekondari zilizopo kata hiyo zinakabiliwa na matatizo lukuki ikiwemo upungufu wa vyumba vya madarasa hali inayosababisha wanafunzi kati ya 140 hadi 160 kusomea katika darasa moja.
.
“Shule za kata yangu kwa kweli zinakabiliwa na changamoto nyingi, kwa mfano Shule ya Msingi ya Majani ya Chai ina vyumba vya madarasa nane wakati wanafunzi waliopo ni 2,200,  Shule ya Msingi ya Minazi Mirefu madarasa yake yaliyopo ni machakavu pia hayatoshelezi,”alisema Kaluwa.

Kaluwa alisema jitihada nyingine zilizofanywa katika kutafuta pesa kwa ajili ya kuziboresha shule hizo ambapo Machi 17 mwaka huu kuliitishwa matembezi ya hisani yaliyoongozwa na mke wa Rais Mama Salma Kikwete.

Aliongeza kuwa katika hafla hiyo kiasi cha shilingi milioni 15 kilichangwa na wadau mbalimbali ambapo kati ya hizo Sh.Milioni 3 zilitolewa na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na Clouds Media Group ambao walitoa shilingi milioni moja na wanafunzi kadhaa wa shule za msingi na sekondari.


Mbunge wa Jimbo la Segerea Dk.Makongoro Mahanga aliwashukuru wadau waliojitokeza kuchangia kata hiyo ambayo ipo katika jimbo lake na kuwataka wadau wengeni kuchangia kata zingine ili kukabiliana na matatizo hayo katika shule mbalimbali.
 
 

Baraza la Sanaa (BASATA) lawapa somo waandaaji wa Epic Bongo Star Search 2012


Na Mwandishi Wetu
BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) limeendesha semina ya siku moja kwa majaji wa shindano la Epic Bongo Star Search 2012 kwa kuwataka kuzingatia maadili ya kazi zao.
  Akitoa somo kwa majaji hao mratibu wa matukio wa Basata Malimi Mashili aliwataka majaji hao kutambua kuwa asilimia kubwa  ya washiriki wanategemea zaidi msaada wao katika kukuza vipaji.
 Mashili aliwataka majaji hao kutambua kuwa mazingira waliyotoka washiriki na kuangalia namna ya kuwasaidia kulingana na mikoa yao kwa kuwa wapo ambao wana vipaji lakini wanatatizwa na suala la kuyazoea mazingira.
  Alisema kuwa kwa kuwa mwaka huu EBSS itaruhusu washiriki wa miaka 16 hivyo ni vema zaidi wakazingatia suala la sauti kulingana na umri wa mshiriki sababu watakuwepo wenye sauti za kitoto pia.
  Pia aliwataka majaji hao kuhakikisha kuwa hawatoi aina yoyote ya upendeleo na wala kuwa karibu zaidi na baadhi ya washiriki wa shindano hilo.
  Pia alisisitiza kuwa majaji wanalo jukumu kubwa la kuwaelekeza namna ya kuimba, kuvaa, kujiheshimu na usafi wa mwili pia.
  “Hiii ni semina ya kuwekana sawa tu kwa kuwa hili shindano lipo kwa muda mrefu na majaji mmekuwa mkifanya vema, kwa niaba ya BASATA napenda kuchukua muda huu kuwataka muwe makini katika kuzingatia maadili haya niliyoyasema na hata mengine pia”alisema Mashili.Naye Mkurugenzi wa Berchmark Production inayoandaa shindano hilo Ritha Paulsen alisema kuwa semina hiyo ni muhimu kwa majaji kwa kuwa  muda mzuri wa kukumbushana mambo muhimu yahusuyo muziki.
  Epiq Bongo Star Search mwaka huu inaanzia mkoani Dodoma Juni 16 katika ukumbi wa Royal Village.
  Majaji wa shindano hilo waliohudhuria ni pamoja na Jaji Mkuu Ritha Paulsen, Master Jay, Salama  pamoja na mratibu wa EBSS kutoka Basata Vicky Temu.
 
 
 
 

No comments:

Post a Comment