Saturday, May 12, 2012

Taswira Za Mkutano Wa CHADEMA Wilayani Same,Wazidi Kuvuna Wanachama Wapya Kutoka CCM na Katibu Mkuu wa Chama Cha TLP Same Ajiunga na Chadema

  James Ole Millya akihutubia
 Katibu Mkuu wa TLP Same, Heriel Msolo(kulia) akirudisha kadi jana Mbele ya Mwenyekiti wa Baraza la Vijana BAVICHA, Ngd Jhon Heche(wa pili kushoto)na Aliekuwa mbunge wa Arusha Mjini(CHADEMA), Godbless Lema(Kushoto)
  Vijana wakigombea ofa ya kadi 10 za Millya
  James Ole Millya akisalimiana na mwanachama wa CCM aliahamia CHADEMA Same jana
  Aliekuwa mbunge wa Arusha Mjini(CHADEMA), Godbless Lema akiwasili Same
  Wananchi wa Same wakigombea foleni ya kupatiwa kadi za CHADEMA jana
-- 
Habari na  Seria Tuma

CHADEMA wanaziara ya kichama Wilayani Same kwa siku nne,kuanzia jana hadi jumatatu chini ya Mwenyekiti wa Baraza la Vijana BAVICHA, Ngd John Heche.

Wana mikutano maeneo tofauti ya Wilaya katika kuimarisha chama hicho.Mkutano wa jana ulifanyikia viwanja vya Kwasakwasa Mjini Same kuanzia saa 9 hadi saa 12 jioni

Viongozi waliohudhuria ni pamoja na aliekuwa mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, Mwenyekiti Bavicha, John Heche, Mweyekiti CHADEMA Kilimanjaro, Augustino Matemu na kiongozi wa vijana Babati, Wilson Mattaka.

Wengine ni James Ole Millya aliekuwa Mwenyekiti UVCCM Arusha, aliekuwa Mjumbe wa NEC CCM kutoka Arusha, Ndg Ally Bananga na aliekuwa Diwani wa Sombetion (CCM). WOte hawa walihamia CHADEMA mapema mwezi huu

Katika mkutano huo kadi nyingi sana zilitolewa na kuasiniwa na John Heche..tena zikigombewa kununua. Lema litoa ofa ya kadi 10 kwa kina mama na Millya nae akatoa ofa ya kuwalipia vijana kumi..

Aliekuwa Katibu Mkuu wa TLP Same, Ndg Heriel Msolo alirudisha kadi ya TLP na kupewa kadi ya CHADEMA na Mwenyekiti wa BAVICHA, John Heche

Lema aliwataka watanzania kutokubali kugwanywa na wanasiasa kwa misingi ya udini na ukabila au ukanda na kueleza kwamba CHADEMA haipiganii maslahi ya kundi lolote katika hayo. Akasema hata yeye hapiganiimaslahi yake binafsi bali ya watanzania.

John Heche aliwataka watanzania kujitokeza kutoa maoni yao kwa tume ya Katiba na kuelekeza kuwa wakatae au wazifanyie mabadiliko makubwa nafasi za uDC au uRC na nyinginezo za kuteuliwa na mtu mmoja. Akadai pia madaraka ya rais ni makubwa na mamabo mengi yameachwa kwa mtu mmoja. hali inayohitaji marekebisho ili kuwe na uwajibikaji wa pamoja..
 
 
 
 
 

Beatrice; Mtanzania aliyeshinda Medali ya Shaba ya Upishi Dernmark katika masomo

Beatrice Stefano Mpangala, 23, mtanzania aliyekuwa akisomea masomo ya Upishi katika chuo cha Elimu ya Juu cha katika Aabenraa nchini Denmark amefaulu vyema masomo yake na kutunukiwa Medali ya Shaba
 Beatrice ambaye ni Binti wa Sophia Mpangala wa Kibaha Mail Moja mkoani Pwani

Beatrice ni chef mwanafunzi katika Hoteli ya  Vojens ya nchini humo na alimaliza mazoezi yake kwa vitendo Hotelini hapo na kutunukiwa Medali hiyo kwa kufanya vyema katika masomo yake.

Kwa hiyo mimi niko tayari kwa changamoto mpya nitakazo kabiliana nazo katika miji mikubwa”, anasema Beatrice, ambaye ubunifu wake katika mapichi umempa tuzo hiyo.

Nae Niels Laursen, ambaye ni Ofisa katika katika Hoteli Vojens alikofanya mafunzo hayo anasema amejisikia fahari sana kwa mtanzania huyo mwenye vipaji lukuki vya upishi na anapasha kuwa ni mara ya kwanza kwa mwanafunzi aliyepita hapo kufanya vyema na kutwaa medali ya Shaba.
 Beatrice akiwa na Niels Laursen
Beatrice Stefano Mpangala, 23 år, bestod svendeprøven som kok på Fagskolen i Aabenraa. Beatrice fik bronzemedalje. Beatrice er kokkeelev på Hotel Vojens. Beatrice afslutter lærlingetiden den 30. november på Hotel Vojens. 

- Så er jeg klar til nye udfordringer gerne i en større by, siger Beatrice, der går ind for kreativ madlavning.

Niels Laursen, vært på Hotel Vojens er naturligvis stolt at sin dygtige kokkeelev og fortæller at det er første gang, at en af hans elever er blevet belønnet med en bronzemedalje.GONGA HAPA kusoma  zaidi  BITE 
 
 
 
 
 

Airtel Yatoa Msaada wa Madawati na Mipira kwa shule za Msingi za Maarifa, Mwangaza na JICA zilizopo Gongolamboto Jijini Dar

Mchezaji wa zamani wa Klabu ya Manchester United ya Uingereza Quinton Fortune, akikabidhi moja ya madawati yaliyotolewa na Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Maarifa Mareitha Mulyalya huku Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Elimu), Mh Kassim Majaliwa akitazama. Kampuni ya Airtel Tanzania ilitoa mipira 30, jesi seti tatu na madawati 40 kwa shule za msingi za Maarifa, JICA na Mwangaza zote za Gongo La Mboto, Dar es Salaam.
Mchezaji wa zamani wa Manchester United ya Uingereza Quinton Fortunewa pili kulia, akionyesha waandishi wa habari (hawako pichani) baadhi ya vifaa vya michezo vitakavyotumika kwenye michuano ya soka ya kimataifa kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 ya Airtel Rising Stars jana kwenye Hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam. Kati ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Technologia Mh. Professa Makame Mbarawa, wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mashindano wa TFF Sandy Kawembe, Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Sam Elangallor na Mkurugenzi Bidhaa Airtel Afrika Obina Justine.
Mchezaji wa zamani wa Klabu ya Manchester United ya Uingereza Quinton Fortune, akipiga mpira kuashiria uzinduzi rasmi wa michuano ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 ya Airtel Rising Stars. Uzinduzi huo ulifanyika jana, Mei 10, kwenye Hoteli ya Sea Clif, jijini Dar es Salaam.
Msanii wa kizazi kipya Ambwene Yesaya maarufu kama AY, akiwatumbuiza wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Maarifa iliyopo Gongo La Mboto nje kidogo Jijini Dar es Salaam wakati Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel ilipotoa msaada wa madawati 30, mipira ya miguu 40 na jezi seti tatu, Alhamisi Mei 10, 2012 ambapo mgeni rasmi alikuwa Naibu Waziri kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mtaa (Elimu) Mh. Kassim Majaliwa. Shule zingine zilizofaindika na msaada ni Maarifa, JICA na Mwangaza zote za Gongo La Mboto, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment