Wednesday, May 16, 2012

TANZANIA YAWA TISHIO INDABA

Naibu Waziri wa Utalii wa Afrika Kusini Bibi Tokozile Xasa (watatu kushoto) pamoja na Kurugenzi Mwendeshaji Biashara na viwanda wa Afrika Kusini Bibi Elizabeth Thabethe  (wa kwanza kushoto) katika picha ya pamoja na baadhi ya waoneshaji kutoka Tanzania wakiongozwa na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania Dk. Aloyce Nzuki (wan ne kushoto) alipotembelea Banda la Tanzania katika maonesho ya INDABA mjini Durban Afrika Kusini.
Na: Geofrey Tengeneza, Durban. 
 
Banda la Tanzania katika maonyesho ya Utalii ya Kimataifa ya INDABA yanayoendelea jijini Durban Afrika Kusini limeendelea kuvutia viongozi na watu wa kada mbalimbali kutoka ndani na nje ya Afrika Kusini wanaotembelea maonyesho hayo.  Miongoni mwa waliotembelea banda hilo shindwa kuzuia hisia zao hususan kwa maelezo na vielelezo vinavyoonesha uzuri na upekee wa vivutio vya utalii vya Tanzania na shughuli za utalii zinavyoendeshwa nchini ni Naibu Waziri wa Utalii wa Afrika Kusini Bibi Tokozile Xasa na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Viwanda na Biashara la Afrika Kusini Bibi Elizabeth Thabethe  ambao kwa pamoja walitembelea Banda la Tanzania na kujionea vielelezo mbalimbali sambamba na kupata maelezo yaliyowafurahisha sana kuhusu utalii wa Tanzania kwa ujumla.
 
Akizungumza na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania Dk Aloyce Nzuki na waoneshaji wa Tanzania kwa ujumla Naibu huyo waziri alifurahishwa na kuvutiwa na jinsi Tanzania kupitia Bodi ya Utalii ilivyojipanga katika kuitangaza Tanzania duniani  na jinsi ambavyo Tanzania imekuwa ni mshiriki mzuri wa maonesho ya INDABA na kukiri kuwa Tanzania imekuwa ikitoa changamoto kubwa kwa nchi nyingine wanachama wa SADC katika sekta ya Utalii. “Tanzania ni nchi tishio katika sekta ya utalii miongoni mwa nchi za SADC, ni nchi inayonivutia sana “ alisema Bibi Tokozile Xasa
 
Jumla ya makampuni 49 kutoka sekta binafsi na taasisi sita za serikali zinashiriki katika maonesho hayo ambayo ni makubwa kuliko yote barani Afrika. Maonesho haya hufanyika kila mwaka jijini Durban Afrika Kusini. Katika maonesho kama haya mwaka jana Banda laTanzania lilitunukiwa tuzo ya kuwa Banda Bora kuliko yote katika maonesho hayo miongoni mwa nchi za SADC.
 
 
 

MKUTANO WA KIMATAIFA WA MABADILIKO YA TABIANCHI WAFANYIKA UJERUMANI

 Bi. Christiana Figeres, Executive Secretary wa  United Nations Framework Convention on Climate Change (UNFCCC) akifungua mkutano  wa kimataifa wa sayansi na taaluma wa mabadiliko ya tabia nchi, Mjini Bonn Ujerumani.
 Pichani Kulia, Bw Richard Muyungi Mkurugenzi  Msaidizi wa Idara ya Mazingira Ya Ofisi wa Makamu wa Rais, ambae Pia ni mwenyekiti wa Dunia wa kamati ya sayansi na Taaluma ya Mabadiliko ya Tabia Nchi, pamoja na washiriki wengine katika ufunguzi wa mkutano wa kimataifa wa mabadiliko ya Tabia nchi unaoendela mjini Bonn Ujerumani
Mbele Kulia, Bwana Alfonce Bikulamchi, Afisa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais akifuatilia kwa umakini ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Sayansi na Taaluma wa masuala ya mabadiliko ya Tabia Nchi unaondelea Mjini Bonn Ujerumani.  Picha na Evelyn Mkokoi, Bonn
 
 

MAMA SALMA AZINDUA 'OKOA MAISHA YA MAMA NA MTOTO'

Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo Mama Salma Kikwete akifuatana na Waziri wa Afya Mheshimiwa Dr. Hussein Mwinyi (kushoto),na Mkurugenzi wa Amref Dr. Festus Lakko (kulia) wakiangalia machapisho mbalimbali yanayohusiana na afya ya mama na mtoto kutoka shirika la Amref wakati wa uzinduzi rasmi wa 'Okoa maisha ya mama na mtoto. Changia mafunzo ya wakunga', au, stand up for African women. Uzinduzi huo ulifanyika katika viwanja vya Mnazi mmoja tarehe 15.5.2012.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiangalia zawadi ya saa aliyopewa na uongozi wa Amref yenye ujumbe wa 'stand up for African women' mara baada ya kuzindua rasmi kampeni ya kuchangia mafunzo ya wakunga ili kuokoa maisha ya mama na mtoto barani Africa yaliyofanyika Mnazi mmoja jijini Dar tarehe 15.5.2012.
Mwenyekiti wa WAMA na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisaini katika kompyuta kuashiria uzinduzi rasmi wa kampeni ya 'Stand up for African women' inayoratibiwa na Shirika la Amref. Uzinduzi huo ulifanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam tarehe 15.5.2012. PICHA NA JOHN  LUKUWI 
 
 

Jukwaa la Vyombo vya Habari Afrika lilivyorindima Uturuki


Mhariri Mkuu wa gazeti la Jambo Leo, Willy Edward akiwasilisha mada katika mkutano wa Jukwaa la Vyombo vya Habari Afrika na Uturuki kuhusu 'Vyombo vya Habari kama kichocheo cha ushindi wa vita dhidi ya migogoro na ugaidi' mjini Ankara, Uturuki wiki iliyopita. Mkutano huo ulioandaliwa na ofisi ya Waziri Mkuu, ulishirikisha wawakilishi wa vyombo vya habari na wadau wengine kutoka nchi 54 za Afrika.

Mhariri Mkuu wa gazeti la Jambo Leo, Willy Edward (kushoto) akipokea tuzo maalumu kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Jamhuri ya Uturuki (Idara ya Habari na Maelezo), Murat Karakaya iliyotolewa kwa niaba ya Naibu Waziri Mkuu Uturuki, Bulent Arinc aliyemwakilisha Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Recep Tayyip Erdogan, baada ya kuwasilisha mada katika mkutano wa Jukwaa la Vyombo vya Habari Afrika na Uturuki kuhusu 'Vyombo vya Habari kama kichocheo cha ushindi wa vita dhidi ya migogoro na ugaidi' mjini Ankara, Uturuki wiki iliyopita. Mkutano huo ulioandaliwa na ofisi ya Waziri Mkuu, ulishirikisha wawakilishi wa vyombo vya habari na wadau wengine kutoka nchi 54 za Afrika.
Naibu Waziri Mkuu Uturuki, Bulent Arinc akifungua mkutano wa Jukwaa la Vyombo vya Habari Afrika na Uturuki mjini Ankara, Uturuki wiki iliyopita. Mkutano huo ulishirikisha wawakilishi wa vyombo vya habari na wadau wengine kutoka nchi 54 za Afrika.
Mhariri wa Habari wa gazeti la Nipashe Jumapili, Beatrice Bandawe(wa pili kushoto) akifuatilia mkutano wa Jukwaa la Vyombo vya Habari Afrika na Uturuki mjini Ankara, Uturuki wiki iliyopita.
Mkurugenzi wa Raia Mwema aliyepata pia kuwa MhaririMtendaji wa gazeti hilo na Kampuni ya New Habari Corporation 2006, John Bwire (kushoto) na Mhariri wa Makala wa Habari Leo, Selemani Nzaro wakifuatilia mkutano wa Jukwaa la Vyombo vya Habari Afrika na Uturuki mjini Ankara, Uturuki wiki iliyopita. Mkutano huo ulioandaliwa na ofisi ya Waziri Mkuu Uturuki, ulishirikisha wawakilishi wa vyombo vya habari na wadau wengine kutoka nchi 54 za Afrika.
Profesa, Dk. Mohamed Bakari, raia wa Kenya anayefundisha Chuo Kikuu cha Fatih nchini Uturuki, akipokea tuzo maalumu iliyotolewa kwa niaba ya Naibu Waziri Mkuu Uturuki, Bulent Arinc baada ya kuwasilisha mada katika mkutano wa Jukwaa la Vyombo vya Habari Afrika na Uturuki kuhusu 'Afrika ya Leo: Sera za Siasa, Uchumi na Mambo ya Nje' mjini Ankara, Uturuki wiki iliyopita. Mkutano huo ulishirikisha wawakilishi wa vyombo vya habari na wadau wengine kutoka nchi 54 za Afrika.
Baadhi ya washiriki wakifuatilia wakati Mhariri Mkuu wa gazeti la Jambo Leo, Willy Edward (mbele kwenye video) akiwasilisha mada katika mkutano wa Jukwaa la Vyombo vya Habari Afrika na Uturuki kuhusu 'Vyombo vya Habari kama kichocheo cha ushindi wa vita dhidi ya migogoro na ugaidi' mjini Ankara, Uturuki wiki iliyopita. Mkutano huo ulioandaliwa na ofisi ya Waziri Mkuu Uturuki, ulishirikisha wawakilishi wa vyombo vya habari na wadau wengine kutoka nchi 54 za Afrika

 
 

No comments:

Post a Comment