Saturday, May 26, 2012

TAASISI YA WANAFUNZI WANAOSOMA SHAHADA YA KWANZA YA SOSHOLOJIA YA CHUO KIKUU CHA DODOMA (UDOMSSO) YAPATA VIONGOZI WAPYA LEO MCHANA

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Kutoka Mwaka wa 1 alipokua akitoa maelekezo ya nini kifanyike kabla ya Zoezi la Kupiga kura na Kutangaza washindi
 Mgombea wa Nafasi ya Mwenyekiti katika taasisi ya wanafunzi wanaosoma Shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO) Bw Edgar Kelvin ambaye anasomma mwaka wa 2 alipokua akinadi sera zake kabla zoezi la kupiga alijaanza
Mgombea wa pili wa nafasi ya Mwenyekiti katika taasisi ya Wanafunzi wanaosoma shahada ya kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO) Bi Loyce Haule ambaye anasoma mwaka wa 2 akinadi Sera zake
Mgombea wa Tatu wa Nafasi ya Mwenyekiti katika taasisi ya Wanafunzi wanaosoma shahada ya kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO) Bw Mwakindaga Emmanuel ambaye anasoma mwaka wa 2 akinadi sera zake
Mgombea Wa Nafasi ya Makamu Mwenyekiti katika taasisi ya Wanafunzi wanaosoma shahada ya kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO) Bw Mtono Juma ambaye amepita bila kupingwa kutoka na kuwa mgombea pekee wa nafasi hiyo na ni mwanafunzi kutoka mwaka wa kwanza
Mmoja wa Wanafunzi Kutoka Mwaka wa 3 Sophia Mkingiye akiuliza Maswala mara baada ya Wagombea kumaliza kunadi sera wakati walipokua wakiomba kura kwa wajumbe na wanachama
Mwanafunzi wa Mwaka wa 2 ambaye anasoma shahada ya kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma Bi Hadija Hassan alipokua akiuliza swali wakati kwa wagombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanafunzi wanaosoma shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma Wakati Wa Uchaguzi wa Kuwachagua Viongozi wapya wa Nafasi mbalimbali Katika Taasisi hiyo Mchana wa Leo
Baadhi ya wanafunzi wanaosoma Shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma waliohudhuria katika uchaguzi wa kuchagua viongozi wa taasisi ya Wanafunzi wanaosoma Shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO) katika uchaguzi uliofanyika ndani ya Chuo Kikuu Cha Dodoma mchana wa leo
Zoezi la Kuesabu kura likiendelea hapo 
Mwenyekiti aliyemaliza muda wake Bw Emmanuel Misungwi Alipokua akitoa Shukrani wa wanachama na wadau wa taasisi hiyo Kwa Kipindi Chote alichokua madarakani kwa mazuri na mabaya ambayo taasisi imepitia na kushukuru kwa wanachama kushiriki zoezi la kupiga kura na kupata viongozi wapya wa Taasisi ya Wanafunzi wanaosoma Shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOMSSO)
Baadhi ya Viongozi wapya wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi waliomaliza muda wao leo mara baada ya zoezi la kupiga kura kumalizika na hatimaye kuwapata viongozi wa taasisi ya wanafunzi wanasoma shahada ya kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma mchana wa leo
Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanafunzi wanaosoma Shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma aliyemaliza muda wake leo Mh Emmanuel Misungwi (Katikati) Akiwa katika Picha ya Pamoja na Mwenyekiti mpya wa Taasisi hiyo Mh Edgar Kelvin (Wa kwanza kulia) na Aliyekuwa Mwenyekiti Wa UChaguzi Wa Kwanza Kushoto


FINA REVOCATUS AIBUKA KIDEDEA NA KUWA REDD'S MISSS IFM 2012

Washiriki walioingia kwenye tano Bora.

Mshindi wa Redd's Miss IFM 2012,Fina Revocatus (katikati) akiwa na Mshindi wa Pili,Jane Augustino (kushoto) na wa Tatu Theresia Issaya muda mfupi baada ya kumalizika kwa shindano lao hilo lililofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa Hoteli ya Blue Peal,Ubungo Jijini Dar.

Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva,Diamond akifanya vitu vyake wakati wa onyesho hilo la urembo  lililofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa Hoteli ya Blue Peal,Ubungo Jijini Dar.

RAIS KIKWETE KUFUNGUA MKUTANO WA AFDB AMBAO UTAGARIMU BILIONI 12

Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya mkutano wa (AFDB) Bw. Ngosha Magonya  katikati akiongea na waandishi wa habari mapema leo jijini Arusha.
Baadhi ya wanakamati wa kamati ya maandalizi ya mkutano wa AFDBwakiwa katika viwanja vya AICC jijini Arusha leo.

NA GLADNESS MUSHI WA FULLSHANGWE-ARUSHA
 Benki ya maendeleo ya Afrika (AFDB)inatarajia kutumia kiasi cha Shilingi bilioni 12 katika mkutano wake unaoanza Jumatatu jijini Arusha na kufunguliwa na Raisi Jakaya Kikwete  huku kiasi cha fedha hizo zikitumika kukarabati Kumbi mbalimbali za jengo la Kimaitaifa la ukumbi wa AICC kwa kuwa baadhi ya kumbi za jengo hilo zinaonekana kupitwa na wakati kutokana na utandawazi uliopo kwa sasa ndani ya nchi zilizoendelea
Akizungumza jijini hapa na waandishi wa habari mwenyekiti wa kamati ya kitaifa ya mkutano wa benki ya AFDB kwa mwaka 2012 Bw Ngosha  Magonya  ambapo alisema kuwa mkutano huo utakuwa na faida kubwa sana

Alifafanua kuwa kupitia mkutano huo ambao utaanza Jumatatu ijayo utakuwa na faida kubwa sana kwa jiji la Arusha kwa kuwa hata kiwango cha uchumi kitaaimarika sana kwa kuwa wageni mbalimbali kutoka katika maeneo ya nchi mbalimbali duniani watabadilishana hata uzoefu

“kwa kipindi hiki ambacho kuna mikutano ndani ya jiji la Arusha tunatarajia kuwepo na utoafuti wa khali ya juu sana hasa katika mchakato wa uchumi na kwa hali hii pia tunatarajia hata kufanya maendeleo mbalimbali  ikiwemo kufanya marekebisho kwa jengo la kimataifa la AICC”alisema bw Magonya

Katika hatua nyingine alifafanua kuwa mbali na kuweza kuimarisha uchumi wa mkoa wa Arusha pia wanatarajia kutumia fursa mbalimbali za kuhakikisha kuwa wanakutanisha wafanyabiashara mbalimbali huku malengo yakiwa ni kuendeleza uchumi kwa walengwa.

Pia alifafanua kuwa mbali na kuweza kuwasaidia wafanyabiashara hao katika michakato ya kukuza uchumi pia benki hiyo ina mikakati mbalimbali ya kuendeleza barabara ambazo zitaweza kutumika kama njia ya mawasiliano hapa Tanzania hali ambayo nayo itachangia kwa kiwango kikubwa sana hata kuimarisha uchumi wa nchi ya Tanzania

Aliongeza kuwa hapo awali benki hiyo ilikuwa imeshajenga barabara ya Arusha –Namanga kwa sasa ana mpango wa kujenga barabara ya Arusha – Holile ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro hali ambayo itachangia sana maendeleo hasa ya mawasiliano

Alimalizia kwa kusema kuwa wafanyabiashara hasa wa mkoa wa Arusha wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanatumia vema fursa za mkutano huo ili kuweza kuimarisha biashara zao za kila siku.
 
 

TAIFA KATIKA TASWIRA:Marais wastaafu wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi (kulia), Benjamin Mkapa (kushoto), Rais mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume (katikati) sambamba na marais wengine wakiwasili kwenye Viwanja vya Chuo Kikuu cha Witwatersrand, Johannesburg, Afrika Kusini

 
Marais wastaafu wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi (kulia), Benjamin Mkapa (kushoto), Rais mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume (katikati) sambamba na marais wengine wakiwasili kwenye Viwanja vya Chuo Kikuu cha Witwatersrand, Johannesburg, Afrika Kusini kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa kujadili maendeleo ya matumizi ya nishati, Karne ya 21 kwa nchi za Afrika. (Na Mpigapicha Wetu).

No comments:

Post a Comment