Wednesday, May 30, 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AMKARIBISHA MAKAMU WA RAIS WA IRAN KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU

 

 

 

 


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkaribisha Makamu wa Rais wa Iran, Mhe. Mohammad Reza Rahimi, wakati alipowasili  Ofisini kwake Ikulu Dar es Salaam kwa mazungumzo leo Mei 30, 2012. Makamu wa Rais wa Iran  amewasili nchini kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku tatu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,  akipokea zawadi kutoka kwa Makamu wa Rais wa Iran, Mhe. Mohammad Reza Rahimi, baada ya  kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Makamu Ikulu Dar es Salaam, leo Mei 30,  2012, (kulia) ni Waziri wa Kazi wa Iran, Sheykhales Lam (kushoto) ni Mkarimaniwa Makamu wa  Rais wa Iran.Makamu wa Rais wa Iran amewasili nchini kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku  tatu.
Makamu wa Rais wa Iran, Mhe. Mohammad Reza Rahimi, akiweka saini katika kitabu cha  Ofisi ya Makamu wa Rais wa Jmahuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,  (katikati) wakati alipofika Ofisini kwake kwa ajili ya mazungumzo leo Me 30, 2012. Kulia  ni Waziri wa Kazi wa Iran, Sheykhales Lam. Makamu wa Rais wa Iran amewasili nchini kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku tatu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na Makamu wa Rais wa Iran, Mhe. Mohammad Reza Rahimi, wakati alipofika Ofisini  kwake Ikulu Dar es Salaam leo, Mei 30, 2012 kwa ajili ya mazungumzo. Makamu wa Rais wa  Iran amewasili nchini kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku tatu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Makamu wa Rais wa Iran, Mhe. Mohammad Reza Rahimi, baada ya kumaliza  mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Makamu Ikulu Dar es Salaam, leo Mei 30, 2012.  Makamu wa Rais wa Iran amewasili nchini kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku tatu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Makamu wa Rais wa Iran, Mhe. Mohammad Reza Rahimi, wakiwa katika mazungumzo maalum,  katika ukumbi wa Hoteli ya Hyatt Kilimanjaro Dar es Salaam leo Mei 30, 2012. Makamu wa  Rais wa Iran amewasili nchini kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku tatu.Picha na Muhidin  Sufiani-OMR

Airtel yaongeza zawadi ya Tsh 143 m/-katika promosheni ya Nani Mkali

Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando akitangaza  kuongeka kwa  zawadi ya  hadi Tsh 143 m/-katika promosheni ya Nani Mkali itakayoendelea kwa muda wa miezi miwili zaidi, kulia ni Afisa Uhusiano wa Airtel Bi Dangio Kaniki akifuatilia wakati wa mkutano wa waandishi wa habari (hawapo pichani) Ili kushiriki promosheni andika  neno “Mkali” tuma kwenda  15656 bure. Baada ya hapo atatumiwa maswali na kila atakapo toa jibu sahihi atapata pointi 20 na jibu lisilo sahihi pointi 10.Kila ujumbe wenye jibu utatozwa shillingi 350 pamoja na kodi.
 
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imeongeza muda kwa wateja wake kuendelea kucheza promosheni yake kabambe ya Nani mkali ambayo ilianza miezi mitatu iliyopita na kuwafaidisha zaidi ya wateja 90 wa Airtel waliojishindia jumla ya miliono 217 kwa mgawanyo wa kuanzia milioni 1 kila siku, milioni 3 kila wiki na milioni 30 kwa washindi wa mwezi 
 Akiongea na waandishi wa habari leo Meneja uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando alisema promosheni hii imekuwa na faida kwetu Airtel wateja wetu waliokuwa wakishiriki wameifurahia na ndio maana leo tumeamua kuongeza zawadi na muda wa promosheni ya Nani Mkali

Hivyo promosheni yetu inaongezwa muda wa miezi miwili huku zawadi zitakazo toka ni pesa taslim Jumla ya ya shilingi milioni 143 katika mgawanyo wa kuanzia shilingi  milioni 1 kila siku-washindi 52, milioni 3 kila wiki –washindi 7,na milioni 30 kwa kila mwezi  itatoka kwa washindi 2. 
 
 
 

Mkataba wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 22.1 kutoka Wete hadi Chakechake kisiwani Pemba wasainiwa

Waziri wa Fedha Dkt William Mgimwa (kushoto) akibadilishana hati ya mkataba wa mkopo nafuu na Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Waarabu inayojishughulisha na Maendeleo ya Uchumi ya Afrika (BADEA) Bw. Abdelaziz Khelef (kulia)leo mjini Arusha wa mradi wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 22.1 kutoka Wete hadi Chakechake kisiwani Pemba. Mradi huo utagharimu shilingi bilioni 15.
Waziri wa Fedha Dkt William Mgimwa (kushoto) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari jana mjini Arusha mara baada ya kubadilishana hati ya mkataba wa mkopo nafuu na Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Waarabu inayojishughulisha na Maendeleo ya Uchumi ya Afrika (BADEA) Bw. Abdelaziz Khelef (kulia) wa mradi wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 22.1 kutoka Wete hadi Chakechake kisiwani Pemba. Mradi huo utagharimu shilingi bilioni 15.
Waziri wa Fedha na Mipango Ofisi ya Rais Yusuf Omar Mzee (kushoto) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari jana mjini Arusha juu ya umuhimu wa barabara mpya inayotarajiwa kujengwa kutoka ChakeChake hadi Wete kisiwani Pemba mara baada ya Tanzania na  Benki ya Waarabu inayojishughulisha na Maendeleo ya Uchumi ya Afrika (BADEA) kusaini mkataba wa mkopo wa masharti nafuu wa mradi wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 22.1. Kulia ni Waziri wa Miundombinu ,Mawasiliano na Uchukuzi wa Serikali ya Zanzibar Hamad Masoud 
Naibu Waziri wa Fedha Saada Salum  (katikakati) akibadilishana mawazo na Msemaji wa Wizara ya Fedha Bi. Ingiahedi Mduma(kushoto) wakati wa mapumziko baada ya mikutano mbalimabli inayoendelea mjini Arusha ya Benki ya Maendeleo ya Afrika(AfDB). Kulia ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango ya Zanzibar Amina Khamis Shaaban.

Rais Jakaya Kikwete Afanya Mazungunzo na Rais Allasane Ouattara wa Ivory Coast Jijini Arusha

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais  Allasane Ouattara  wa Ivory Coast wakitembea kwa miguu kuelekea kwenye sehemu waliyotengewa kufanyia mazungumzo rasmi katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha leo May 30, 2012 ambako Rais huyo wa Ivory Coast amefika kuhudhuria mkutano wa afDB ambao unbafunguliwa rasmi kesho na Rais Kikwete katika ukumbi wa AICC. Katika maongezi yao Rais Kikwete amesema Tanzania inaunga mkono juhudi za Ivory Coast za kutaka kurejesha nchini humo makao makuu ya afDB ambayo yamehamia Tunisia kutokana na vurugu zilizotokea Abidjan baada ya uchaguzi mkuu mwaka jana.
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais  Allasane Ouattara  wa Ivory Coast wakiangalia shamba la kahawa wakati wakielekea  kwenye sehemu waliyotengewa kufanyia mazungumzo rasmi katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha leo May 30, 2012 ambako Rais huyo wa Ivory Coast amefika kuhudhuria mkutano wa afDB ambao unbafunguliwa rasmi kesho na Rais Kikwete katika ukumbi wa AICC. Katika maongezi yao Rais Kikwete amesema Tanzania inaunga mkono juhudi za Ivory Coast za kutaka kurejesha nchini humo makao makuu ya afDB ambayo yamehamia Tunisia kutokana na vurugu zilizotokea Abidjan baada ya uchaguzi mkuu mwaka jana.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais  Allasane Ouattara  wa Ivory Coast wakiwa katika mazungumzo rasmi katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha leo May 30, 2012 ambako Rais huyo wa Ivory Coast amefika kuhudhuria mkutano wa afDB ambao unbafunguliwa rasmi kesho na Rais Kikwete katika ukumbi wa AICC. Katika maongezi yao Rais Kikwete amesema Tanzania inaunga mkono juhudi za Ivory Coast za kutaka kurejesha nchini humo makao makuu ya afDB ambayo yamehamia Tunisia kutokana na vurugu zilizotokea Abidjan baada ya uchaguzi mkuu mwaka jana.Picha na IKULU

Mbunge wa Bumbuli(CCM)January Makamba Apeleka Umeme Kata ya Mgwashi Kwa Mara ya Kwanza

  Mbunge wa bumbuli(CCM)na Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia Mh January Makamba akihutubia wananchi wake(wapiga kura)kata ya Mgwashi Jimboni kwake Bumbuli,Kwa mara ya kwanza kata hii imepata umeme. Mradi wa maji wa shilingi bilioni moja nukta sita nao karibu utaanza utekelezaji wake.
  Mbunge wa bumbuli(CCM)na Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia Mh January Makamba akilakiwa na wapiga kura wake muda mfupi baada ya kumaliza mkutano wake kata ya mgwashi Bumbuli Mei 28,2012,Kata ya Mgwashi, Bumbuli Mei 28, 2012.Kwa mara ya kwanza kata hii imepata umeme. Mradi wa maji wa shilingi bilioni moja nukta sita nao karibu utaanza utekelezaji wake.

WAREMBO MISS DAR INTERCOLLEGE WAJIFUA VILIVYO LAMADA HOTEL

 Washiriki wa shindano la kumtafuta Malkia wa Miss Dar Intercollege wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa mazoezi yao yanayofanyika kwenye hoteli ya Lamada iliyoko Ilala jijini Dar es salaam jana jioni, warembo hao kila mmoja kwa wakati wame wamejitapa kufanya vizuri katika shindano hilo na kuibuka na ushindi.
 Mwalimu wa warembo mwanaoshiriki katika shindano la Miss Dar Inter College Mrarylydia Bonoface akiwaelekeza jambo wakati wa mazoezi yao jana yanayofanyika kwenye hoteli ya Lamada Ilala jijini Dar es salaam.
Mratibu wa shindano hilo Dina Ismail na mmiliki wa blogu ya www.mamapipiro.blogspot.com akieleza jambo wakati wa mazoezi hayo, na kuwaasa warembo hao kuwa na nidhamu katika mazoezi jambo ambalo litawafanya kuzingatia mambo muhimu watakayoelekezwa na mwalimu wao.
 
 

No comments:

Post a Comment