Thursday, May 24, 2012

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad Akabidhi Bendera Ya Zanzibar Watoto Wanaowawakilisha Watoto Wenzao Mayatima Wakiwa na Viongozi Wao Wanaokwenda nchini Uturuki Kuiwakilisha Zanzibar

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akiwakabidhi bendera ya Zanzibar, Watoto wanaowawakilisha Watoto wezao Mayatima wakiwa na Viongozi wao wanaokwenda nchini Uturuki kuiwakilisha Zanzibar katika Kongamano la Kimataifa la Kuadhimisha Siku ya Watoto Yatima litakalofanyika mjini Istambul Uturuki kuanzia tarehe 28/05 hadi 03/06/2012. na kuwajumuisha Watoto wanaotoka  Nchi mbalimbali Nduniani kushiri katika Kongamano hilo.Picha na Salmin Said,-Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa  Rais Zanzibar
 
 

Waumini wa madhehebu ya Hindu kutoka Tanzania, Kenya, Afrika Kusini, Botswana, India na Uingereza wakiandamana kwenye mitaa mbalimbali ya Jiji la Arusha

Waumini wa madhehebu ya Hindu kutoka Tanzania, Kenya, Afrika Kusini, Botswana, India na Uingereza wakiandamana kwenye mitaa mbalimbali ya Jiji la Arusha kuashiria ufunguzi wa hekalu lao la Swaminarayan Mandir jana. (Picha na Marc Nkwame).
 
 

UBINGWA WA SIMBA KUSHEREHEKEWA DAR LIVE MEI 27

 Kombe la Ubigwa wa Simba ambalo wapenzi watapata nafasi ya kupiga nalo picha siku ya sherehe hizo ndani ya Dar Live.
      Kamwaga akiwa  na  kombe la ubingwa.
  Nahodha wa  Simba, Juma Kaseja,  akielezea  sherehe hiyo.
  Mpiga picha wa Global Publishers, Issa Mnally (kushoto) akiwa amebeba kombe hilo na mmoja wa wazee wa Simba, Juma Issa Matali.
 Mratibu wa Burudani wa Ukumbi wa Dar Live, Juma Mbizo (kushoto) akiongea na waandishi juu ya sherehe hizo.
      Ezekiel Kamwaga (kulia) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani).
    Juma Kaseja akiwa na makombe mbalimbali ambayo Simba wameyatwaa miaka ya nyuma na sasa.
 Waandishi wa habari wakiwa kazini katika hafla hiyo. 
 ----
KLABU  ya soka ya Simba ya jijini Dar es Salaam imepanga kufanya sherehe kubwa ya kutwaa ubingwa wa soka wa Ligi Kuu ya Vodacom katika Ukumbi wa Taifa wa Burudani wa Dar Live siku ya Mei 27, Jumapili, wiki hii.

Akiongea na waandishi wa habari leo mchana, Ofisa Habari wa klabu hiyo, Ezekiel Kamwaga,  alisema kuwa wameamua kufanya sherehe hizo ndani ya ukumbi huo kutokana na ubora wake.

Aidha Kamwaga alisema kuwa siku hiyo pia watawatambulisha wachezaji wapya waliosajiliwa kwa msimu ujao wa ligi na kuwataka wapenzi wa Simba  na wananchi wengine kujitokeza kwa wingi siku hiyo.

No comments:

Post a Comment