Wednesday, March 28, 2012

 

 

 

KIJANA SHABANI ISSA APATIWA MATIBABU NA SASA ANAENDELEA VIZURI.SHUKRANI KWA WOTE WALIOSAIDIA KATIKA HILI.MUNGU AWAZIDISHIE PALE MLIPOTOA

Mtoto Shabani Issa kabla hajaenda kufanyiwa upasuaji

Mnamo Tarehe 15 Mwezi wa 3 2012 Blogu ya Lukaza iliwahi kupost habari ya Kijana Shabani Issa ya kuomba msaada wa Kwenda kupata Matibabu  kutokana na hali yake ya Jicho kuwa na Uvimbe hivi sasa Kijana Shabani Issa anaendelea Vizuri baada ya Kupata matibabu katika Hospitali ya St Benedict Ndanda iliyopo Mkoani Mtwara.Kwa habari ya Kwanza ya Kijana Issa Kuomba Msaada  BOFYA HAPA
Kijana Shabani Issa Akiwa katika Hospitali ya St Benedict iliyopo Mkoani Mtwara baada ya kufanyiwa upasuaji.

Shabani Issa afanyiwa upasuaji jana(27/3/2012) St.Benedict's hospital Ndanda mkoani Mtwara.Anaendelea vizuri mpaka sasa.Namshukuru yeye aliyesimamisha mbingu bila kuweka nguzo kwa mema yake yote ktk shida ya kijana huyu.Nawashukuru wadau walioweza kuchangia kwa namna moja au nyingine.Najua wengine walijua ni uongo natafuta namna ya kuneemesha tumbo na wao nawashukuru pia.Naishukuru hospital ya Ndanda hasa dr.Mathew Ng'onye na Z.A Umbaro kwa jitihada zao ktk kufanikisha upsuaji salama.Mungu awabariki sana
Mtandao Wa Lukaza Blog Unapenda Kutoa shukrani Kwa Wadau Wote Waliowezesha Kijana Huyu Kupatiwa Msaada wa Kupata Matibabu Katika Hospitali ya Mtakatifu Benedict iliyopo Mtwara Mungu Awazidishie pale mlipotoa Kwa Kujali na Kuonyesha Upendo. 
 
 

NAFASI KWA WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA TANO MWAKA 2012


Majina ya wanafunzi waliochaguliwa kuingia kidato cha tano na Chuo cha Usimamizi wa Maji kwa mwaka 2012 yametangazwa na Kamishna wa Elimu ya Sekondari. Pamoja na majina hayo, ripoti pamoja na uchambuzi wa matokeo ya mitihani ya kidato cha nne kwa mwaka 2011 imetolewa. 

icon Wanafunzi waliochaguliwa kuingia kidato cha tano na Chuo cha   Usimamizi wa Maji 2012- Wavulana
icon Wanafunzi waliochaguliwa kuingia kidato cha tano na Chuo cha Usimamizi wa Maji 2012- Wasichana

icon CSEE 2011 - Report and Analysis of the Results 

TANZANIA YASHIRIKI VYEMA KWENYE MAONESHO YA UTALII YALIYOFANYIKA NCHINI UJERUMANI

Baadhi ya wafanyabiashara za utalii toka Tanzania wakiuza bidhaa za Tanzania.
Hawa ni washindi wa mashindano ya watu wenye mustachi yaandi ndeve ndefu zaidi duniani kama wanavyoonekana walipotembelea banda la Tanzania. 

Banda la TTB lilivyokuwa likionekana wakati wa maonesho haya
Bodi ua Utalii Tanzania iliratibu vyema maonesho ya utalii yaliyofanyika nchini ujerumani katika jiji la Berlin kuanzia tarehe 7 – 11 Machi 2012.

Maonesho ya ITB ndio maonesho makubwa duniani yanayowakutanisha wafanya biashara za utalii duniani.

Jumla ya makampuni 59 toka Tanzania ziliweza kuhudhuria kati ya hizi kampuni 31 zilikuwa ni zinazojihusisha na mahoteli (hotel, appartments), kampuni 24 zinazohudumia watalii (tour operatos) na kampuni nne, 39 ndege (Airline carriers).

Katika maonesho haya Bodi ya Utalii iliwaza vyema kutengeneza utalii ambao ni hazina kubwa kwa nchi ya Tanzania.Picha na Habari Kwa Hisani ya Father Kidevu Blogu
 

No comments:

Post a Comment