UJUMBE WETU WA LEO
BASI LA ABOOD LAPATA AJALI ASUBUHI YA LEO MAENEO YA MBEZI
Basi la kampuni ya Abood likiwa
limepinduka maeneo ya Mbezi likiwa linatoka Mkoani Morogoro kuelekea Dar
es salaam asubuhi ya leo.Chanzo cha ajali hii hakikujulikana ila
inasemekana ni kutokana na dereve kuovertake gari mbele na hatimaye
kumshinda na kupinduka.
Wananchi wakitazama jinsi basi la abood lilivyopinduka huku wengine wakiokoa abiria waliopo kwenye basi hilo asubuhi ya leoMAKAMU WA RAIS DKT BILAL ATEMBELEA SHUGHULI ZA UCHIMBAJI WA MAKAA YA MAWE RUANDA (W)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya uchimbaji Makaa ya Mawe, Tancoal, Graeme Robertson, wakati alipotembelea mradi wa Uchimbaji Makaa ya Mawe unaoendelea eneo la Ruanda Wilaya ya Mbinga, wakati akiwa katika ziara yake ya mkoa wa Ruvuma jana.
Ukifanywa utafiti wa kugundua upatikanaji wa makaa ya mawe kabla ya kuanza uchimbaji.
Makaa yakichekechwa na kupatikana makaa bora na mabaki kuwekwa mahala maalum palipoandaliwa ili kuepuka uchafuzi wa mazingira.
Magari
yakiwa mgdini chini yakiendelea na kazi ya uchimbaji wa Makaa ya mawe
hayo ambayo soko lake kubwa limekuwa ni nje ya nchi kama Zambia, Ghana
na kwingineko.
Mke
wa Makamu wa Rais, Mama Asha Bilal (katikati) akiwa na Mke wa Mkuu wa
Mkoa wa Ruvuma (kushoto) na Mke wa Mbunge wa Mbinga, wakati
walipotembelea shughuli hiyo ya uchimbaji.
Sufianimafoto, naye hakusita kupiga picha ya kumbukumbu mahala hapa muhimu kwenye utajiri mkubwa wa Taifa la Tanzania.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani laTaifa (NECTA) Dk. Joyce Ndalichako Azungumza Juu Ya Kufutwa Kwa Mitihani Kwa Baadhi Ya Skuli Zanzibar
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani
la Taifa (NECTA) Dk. Joyce Ndalichako, akizungumza na waandishi wa
habari wa vyombo mbalimbali vilioko Zanzibar matokeo ya kufutwa kwa
mitihani kwa baadi ya Skuli kutokana na kufanya udanganyifu.mkutano huo
umefanyika Hoteli ya Bwawani Zanzibar.
Katibu Mtendaji wa Baraza la
Mitihani la Taifa (NECTA) Dk. Joyce Ndalichako, akionesha ripoti ya
uchunguzi uliofanywa na Taasisi ya Uchunguzi ya Vyombo vya Usalama
kuhusi undanganyifu wa baadi ya miandiko iliotumika katika mitihani ya
watahiniwa wa Kidatu cha Nne.
Katibu Mtendaji wa Baraza la
Matihani la Taifa (NECTA) Dk. Joyce Ndalichoka, akionesho karatasi za
mitihani ambozo zimekuwa na miandiko zaidi ya mmoja na kufanana maneno
ya majawabu.
Mwandishi wa Nipashe Charles
Mwakenja, akiuliza swali katika mkutano huo, Baraza lina mpango gani wa
kupunguza hiyo adhabu waliotowa kwa Wanafunzi.
Mwalim Haji na Mwalim Hassan
wakifuatilia makaratasi ya mitihani ya Watahiniwa wa kidatu cha Nne,
yalioletwa na Katibu Mtendaji waBaraza la Mitihani ikiwa ni vielelezo
kuonesha hakuna Mwanafunzi alioonewa katika adhabu hiyo.
Viongozi wa Chama cha Walimu Zanzibar
, wakiangalia moja ya karatasi za mitihani ambazo zimekutwa na makosa
na kufutiwa watahiniwa wake, wakiwa katika ukumbi wa hoteli ya bwawani.
Waandishi wa habari wakimsikiliza
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Dk Joyce Ndalichoka, akitowa
maelezo ya kufutiwa mitihani watahiniwa wa kidatu cha Nne, wa mwaka
2011.
No comments:
Post a Comment