Wednesday, February 15, 2012

 

 

 

TASWIRA ZA ZAMBIA WALIVYOPOKELEWA



Mabingwa wapya wa soka wa Afrika, Chipolopolo wa Zambia wamepokelewa kwa shangwe katika mji mkuu Lusaka. 
 
Mwandishi wa BBC anasema mashabiki waliokuwa wakisubiri, walilipuka kwa kelele za shangwe, wakati nahodha Christopher Katongo alipotoka kwenye ndege akiwa amelibeba Kombe la dhahabu la Mataifa ya Afrika.

NBC YANUNUA HISA ASILIMIA 10.87 KWENYE KAMPUNI YA MIKOPO YA NYUMBA, TMRC

Washauri wa masuala ya habari NBC kulia ni Redemptus Massanja na Eddie Mhina.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Mortgage Refinance Company Limited (TMRC) Bw Rished Bade kulia na Mkurugenzi mtendaji wa Benki ya NBC Bw. Lawrence Mafuru waliokaa wakiwa katika picha ya pamoja na maafisa kutoka NBC, BOT na TMRC.
Maafisa mbalimbali wakiwa katika mkutano huo leo. 

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Mortgage Refinance Company Limited (TMRC) Bw Rished Bade kulia akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya kukabidhiana hundi ya shilingi bilioni moja kutoka benki ya NBC (katikati)Mkurugenzi mtendaji wa Benki ya NBC Bw. Lawrence Mafuru na kushoto ni Mortgage Finance Specialist kutoka benki kuu Bw. Baraka Munisi.

Mkurugenzi mtendaji wa Benki ya NBC Bw. Lawrence (kushoto) akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi bilioni moja kwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Mortgage Refinance Company Limited (TMRC) Bw Rished Bade katika hafla iliyofanyika kwenye makao makuu ya benki hiyo leo.
 
Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) leo imekabidhi hundi yenye thamani ya Shilingi bilioni moja kwa Kampuni mahususi ya Kutafuta Fedha na Kutoa Mikopo ya Muda Mrefu ya Nyumba iitwayo Tanzania Mortgage Refinance Corporation (TMRC) ikiwa ni kiasi cha kununua hisa za asilimia 10.87 kwenye kampuni hiyo. TMRC ni taasisi ya kifedha inayomilikiwa na mabenki mbali mbali kwa lengo la kusaidia mabenki yaweze kutoa mikopo ya muda mrefu ya nyumba kwa wateja.
Lengo kuu la TMRC ni kusaidia kutoa fedha kwenye soko la kifedha la Tanzania kwa ufanisi, na kuzilenga fedha hizo kwa mabenki wanachama kwa viwango vya ushindani. Hii itawezesha upatikanaji wa makazi kwa watanzania, na pia kuchangia maendeleo ya masoko ya mitaji.
Shughuli hiyo imefanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Benki ya NBC, ikiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Bwana Lawrence Mafuru.
Akizungumza kwenye tukio hilo, Bwana Mafuru alisema: “Tunaamini kuwa fedha hizi zitaiaidia TMRC katika juhudi zake za kuwawezesha Watanzania wapate kumiliki makazi bora. Kitendo hiki kinaonyesha dhamira ya NBC katika kusaidia sekta ya mikopo ya nyumba Tanzania ”
Hundi hiyo imepokewa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa TMRC, Bwana Rished Bade mbele ya viongozi wa ngazi ya juu wa kampuni hiyo pamoja na wawakilishi kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Mwezi Oktoba 2011, NBC pamoja na benki nyingine sita zilisaini mkataba na Shirika la Nyumba Tanzania (NHC) kwa ajili ya kuwawezesha Watanzania kipata makazi bora zaidi
 
 

MISS TANZANIA KUTANGAZA MDHAMINI MPYA WA SHINDANO HILO KESHO

Tarehe 15 Februari 2012 katika ukumbi wa Savannah uliopo katika Jengo la Benjamin Mkapa saa 5.00 asubuhi, kampuni ya Lino International Agency inatarajia kufanya Mkutano na Waandishi wa vyombo mbalimbali vya Habari ili kutangaza mdhamini mkuu mpya wa mashindano ya Miss Tanzania kwa mwaka huu wa 2012.
Taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari hii leo imesema Katika Mkutano huo atatangazwa Mdhamini Mkuu mpya wa Mashindano hayo ya urembo ya Miss Tanzania 2012 hivyo kuashiria mbio mpya za kumpata mwakilishi wa Miss Tanzania katika mashindano ya dunia Miss World.
Mashindano ya Miss Tanzania yalikuwa yakidhaminiwa na kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom kwa muda mrefu mpaka ilipomaliza mkataba wake mwaka jana.

No comments:

Post a Comment