Wednesday, January 25, 2012

 

 

 

 

 

 

TAIFA KATIKA TASWIRA

Wafanyabiashara za zabibu wakiwa wameketi katika kituo cha mabasi yaendayo mikoani mjini Dodoma leo huku  wakisubiri wateja na kuwaita kwaajili ya kuwauzia zabibu.

 

 

Mkuu wa Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma, Betty Mkwasa akimpa chakula moja wa wanafunzi wa shule ya msingi Nguji

Mkuu wa Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma, Betty Mkwasa akimpa chakula moja wa wanafunzi wa shule ya msingi Nguji alipofanya ziara shuleni hapo.Watoto wamekuwa wakipatiwa chakula cha mchana shuleni hapo kila siku ili kuwawezesha wawe wasikivu darasani. (Picha na Sifa Lubasi)

 

Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja Atia Saini Mikataba Mitatu Ya Utafiti Wa Mafuta Nchini

Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja (kushoto) akiwekeana saini na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Motherland Industries Limited kutoka India Bw, V. K. Sood (Kulia) uwekaji saini wa mikataba mitatu ya utafiti wa mafuta nchini, umefanyika leo jijini Dar es Salaam,
Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja (katikati) akiweka saini mkataba wa utafiti wa mafuta nchini kwa kampuni tatu kutoka nje, (kushoto) ni Mkurugenzi mtendaji wa TPDC Bw, Yona Killagane na (kulia) Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Matherland industries LTD kutoka India, Bw. V.K. Sood .(kulia). Mkataba huo umewekwa saini leo kwenye jingo la Wizara ya Nishati na Madini
Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja (kulia) akifafanua jambo wakati wa uwekaji saini wa mikataba mitatu ya uatafiti wa mafuta kutoka kampuni za nje jijini leo DSM (Kulia) ni Kamishna Msaidizi wa Nishati (Petroleum na Gas ) Bw, Prosper Victus
Waziri wa Nishati na Madini Wiliam Ngeleja (kushoto) akibadilisha hati za makubaliano ya utafiti wa mafuta nchini na Mkurugenzi Mtendaji wa kampun i ya Petrobras kutoka Brazil Bw, Samuel Bastos de Miranda (kulia) , hafla hiyo imefanyika leo jijini Dar es Slaam wakati wa hafla ya uwekaji saini wa mikataba mitatu ya utafiti wa mafuta wa kampuni kutoka nje
Kamishna Msaidizi wa Nishati kutoka Wizara ya Nishati na Madini Bw, Prosper Victus (alisimama mbele na Kabrasha) akitoa maelezo ya awali wakati wa uwekaji wa saini mikataba mitatu ya utafii wa mafuta kutoka kampuni za nje leo wakati wa hafla hiyo kwenye jengo la Wizara ya hiyo jijiji Dar es Salaam.Picha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO

 

 

 

 

CHADEMA Yampitisha Mshimbe Mgombea Zanzibar; Yatoa Taarifa Kuhusu Maamuzi ya Kamati Kuu na Kikao Chao Na Rais Jakaya Kikwete

John Mnyika,Mbunge wa Ubungo(CHADEMA)na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi
---
Taarifa ifuatayo inatolewa kwa umma kuhusu Maamuzi ya Mkutano wa Kawaida wa Kamati Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), uliofanyika kwa siku mbili tarehe 20 na 22 Januari 2012 katika Hoteli ya New Africa Jijini Dar es salaam.

Mkutano huo wa kawaida wa Kamati Kuu ulikuwa na ajenda mbalimbali ikiwemo Uteuzi wa mgombea wa uwakilishi wa Jimbo la Uzini na kupitisha mkakati na bajeti ya uchaguzi husika; Taarifa ya Kamati Maalum ya Kamati kuhusu Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 na Taarifa ya Fedha (Mapato na Matumizi ya chama) kwa mwaka 2011.

Kuhusu Uchaguzi wa Uwakilishi katika Jimbo la Uzini:

Katika kikao chake cha tarehe 20 Januari 2012, Kamati Kuu ilimteua Ali Mbarouk Mshimba kuwa mgombea wa uwakilishi wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar katika Jimbo la Uzini kwa tiketi ya CHADEMA.

Aidha, katika kikao chake cha tarehe 22 Januari 2012 Kamati Kuu ya chama imepokea na kujadili mkakati na bajeti ya uchaguzi wa Jimbo la Uzini.

Kamati Kuu imeridhika na maandalizi ya awali ambayo chama kimeyafanya katika Jimbo husika na kuagiza sekretariati ya chama kufanya maandalizi zaidi kwa ajili ya uzinduzi wa kampeni za uchaguzi husika.

Pia, kamati kuu imefanya mapitio ya bajeti na kuweka kikomo cha matumizi ya fedha katika uchaguzi tajwa ili kuhakikisha kwamba kampeni zinafanyika kwa ufanisi na kuendelea kutoa taarifa kwa umma kuhusu utekelezaji wa mikakati husika kwa kuzingatia mahitaji.

Kuhusu Taarifa ya Kamati Maalum kuhusu Sheria ya Mabadiliko ya Katiba:

Kamati Kuu imepokea na kujadili taarifa ya Kamati Maalum kuhusu Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 iliyoundwa na kamati kuu tarehe 20 Novemba 2011.

Pamoja na masuala mengine, Kamati Kuu ilitaarifiwa juu ya yaliyojiri katika mikutano kati ya Kamati Maalum ya CHADEMA na Rais Jakaya Kikwete na serikali tarehe 27 na 28 Novemba 2011 na tarehe 21 Januari 2012.

Aidha kamati kuu ilijulishwa hatua ambazo serikali imefikia katika maandalizi ya kuifanyia marekebisho sheria ya mabadiliko ya katiba ya mwaka 2011 katika Mkutano wa Sita wa Bunge unaotarajia kuanza tarehe 31 Januari 2012.

Kamati Kuu imeamua kwamba Kamati Maalum iendelee kufanya mawasiliano na mashauriano na Rais Kikwete na Serikali kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 inafanyiwa marekebisho ya msingi kabla ya mchakato wa kukusanya maoni kwa mujibu wa sheria husika haujaanza.

Kamati Kuu imeendelea kusisitiza Azimio lake la kikao cha Novemba 20, 2011 kwamba “Ushiriki wa CHADEMA katika mchakato mzima wa kupata Katiba Mpya uliowekwa na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba utategemea utayari wa Serikali ya Rais Kikwete kufanya mabadiliko ya kimsingi katika sheria hiyo kwa lengo la kujenga muafaka wa kitaifa juu ya
mchakato huo”.

Aidha, Kamati Kuu imepokea taarifa kuhusu hatua ambayo imefikiwa na chama katika kufanya mikutano ya ndani katika maeneo mbalimbali ya kuelimisha viongozi, wanachama na wananchi kuhusu upungufu wa sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 pamoja na kupokea maoni kwa ajili ya kuboresha sheria husika.

Kamati Kuu ya chama imeamua kwamba CHADEMA kiendelee kutekeleza azimio la kikao cha Kamati Kuu cha Novemba 20, 2011 la kutoa “kutoa elimu kwa wananchi na wadau wote juu ya ubovu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na juu ya haja ya kuwa na sheria itakayoweka utaratibu bora zaidi wa kuunda Tume Shirikishi ya Katiba kwa lengo la kukusanya maoni ya
wananchi, kuandaa ripoti na Rasimu ya Katiba Mpya, Bunge Maalum la Katiba na usimamizi wa kura ya maoni itakayowezesha wananchi kufanya maamuzi kwa uhuru na kwa haki”.

Kamati Kuu inaendelea kuwaagiza viongozi wote wa chama kama ilivyoelekezwa na Waraka wa Katibu Mkuu Namba 3 wa mwaka 2011, katika ngazi zote kufanya mikutano ya ndani na ya hadhara yenye lengo la kuwaelimisha wananchi juu ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na madhara yake kwa mchakato wa kupata Katiba Mpya na bora kwa nchi yetu kwa
lengo la kuunganisha umma wa watanzania kuweza kufanya mabadiliko ya msingi.

Kuhusu Taarifa ya Fedha (Mapato na Matumizi ya chama) kwa mwaka 2011: Kamati kuu imetaarifiwa kuhusu vyanzo mbalimbali vya mapato ya chama kwa mwaka 2011. Aidha Kamati Kuu imetaarifiwa kuhusu matumizi ambayo yamefanywa na chama katika mwaka 2011 kwa kuzingatia Mpango Mkakati wa chama 2011-2016 na Mpango Kazi wa mwaka 2011.

Kamati Kuu imejulishwa matumizi yaliyofanywa katika utekelezaji wa mipango kwenye vipaumbele mbalimbali ikiwemo upelekaji wa ruzuku majimboni/wilayani/mkoani; ulipaji wa madeni ya uchaguzi mkuu wa 2010 na uwekezaji; uendeshaji wa makao makuu ya chama; utekelezaji wa operesheni za chama na mfuko wa uchaguzi mkuu 2015.

Kamati Kuu imepokea taarifa ya fedha kwa mwaka 2011 na kuagiza sekretariati ya chama kuandaa mkutano maalum kwa ajili ya kuendelea kujadili taarifa husika sanjari na Mpango Kazi wa Chama kwa mwaka 2012; taarifa zaidi kuhusu fedha na mipango itaelezwa baada ya mkutano huo.

Imetolewa tarehe 23 Januari 2012 na:
John Mnyika (Mb) Mkurugenzi wa Habari na Uenezi

 

 

 

 

NAILETA KWENU BLOGU SAFI KABISA YA MITUMBA HALISI BOFYA LINK HAPO

 
Dar es Salaam, Tanzania

Mitumba Halisi inapatikana Dar es salaam Tanzania Mitumba Halisi ni blog ya nguo za kuuza kwaajili ya kina dada na wamama wanaopenda kupendeza. Blog hii inakuletea nguo za kisasa za kila aina na za kila rika, Nguo za wadada kwaajili ya ofisini, kutokea usiku na hata kwaajili ya kuwa casual siku za weekend . Kupitia Blog hii utaweza kuziona nguo na kuagiza popote ulipo Tanzania. KARIBUNI WOTE

KWA KUITEMBELEA BLOGU HII BOFYA HAPA

AU 

http://mitumbahalisi.blogspot.com

No comments:

Post a Comment