Monday, January 23, 2012

 

 

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AZINDUA JENGO LA UTAWALA LA SHULE YA SEKONDARI MNOLELA, AKAGUA UJENZI WA BWENI LA WASICHANA SEKONDARI YA KINENG’ENE-LINDI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Lindi mjini, Salum Baruani, wakati alipowasili kwenye Shule ya Sekondari Mnolela, lindi kwa ajili ya kuzindua Jengo la Utawala la shule hiyo, jana januari 21, 2012, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Lindi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifurahia ngoma ya asili wakati alipowasili kwenye shule ya Sekondari ya Mnolela, alipofika kuzindua Jengo la Utawala la shule hiyo, akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Lindi jana, Januari 21, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifunua kitambaa ikiwa ni ishara ya kuweka jiwe la Msingi katika jengo jipya la Utawala la Shule ya Sekondari Mnolela, iliyopo kijiji cha Luhokwe, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Lindi jana Januari 21, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Lindi, kuelekea kukagua ujenzi wa jengo la Bweni la wasichana shule ya Sekondari ya Kineng’ene, akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Lindi, jana Januari 21, 2012. 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na mkewe, Mama Zakhia Bilal, wakifurahia ngoma ya asili baada ya Makamu kumaliza kuwahutubia wananchi wa Uwanja wa Fisi, mkoani Lindi jana Januari 21. 

 

Edward Lowassa na Zitto Kabwe


Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa akisalimiana na Mbunge wa Kigoma Kaskazini(CHADEMA), Zitto Kabwe kwenye msiba wa Mbunge wa Arumeru na Naibu Waziri wa Fedha Mstaafu Marehemu Jeremia Sumari jana.Picha na Mdau Richard Mwaikenda

 


BASI LA NEW FORCE LAUA STENDI YA MABASI MBEYA

ABIRIA aliyefahamika kwa jina moja la Amina mkazi wa wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya alikufa papo hapo katika ajali iliyotokea juzi usiku katika Kituo cha Mabasi yaendayo Mikoani kutokea Mbeya baada ya basi la New Force kuparamia ukuta wa mgahawa uliopo mkabala na Ofisi za Mabasi ya Kampuni hilo.

Tukio hilo limetokea majira ya saa 5:00 usiku wa Ijumaa ya Januari 20 mwaka huu katika Kituo hicho cha Mabasi yakitokea mikoa mingine.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kondakta wa basi hilo aliyejulikana kwa jina la Januari Kapinga aliingia ndani ya basi hilo lenye namba za usajili T 853 AVQ aina ya Yutong lililokuwa likitokea Dar es Salaam baada ya abiria wote kushuka ndipo alipolikurupua kwa nguvu na kumshinda hatimaye kuparamia ukuta.

Abiria aliyefariki alikuwa safarini kuelekea masomoni mkoani Tabora na wakati gari likiparamia ukuta wa mgahawa huo alikuwa akipata chakula cha jioni

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi imesema licha ya mmoja huyo kupoteza maisha, lakini watano wamejeruhiwa.

Aidha kondakta wa basi hilo alitoroka na kwenda kusikojulikana na juhudi za Jeshi la Polis kumtafuta zinaendelea na hadi sasa dereva wa basi hilo anashikiliwa na Polisi kwa mahojiano zaidi.

Kwa upande wake Noah Mwakatumbula Mwenyekiti wa Kituo cha Mabasi mkoani Mbeya yaendayo mikoani amewataka madereva waliopewa dhamana ya kuendesha vyombo hivyo na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waache mara moja tabia ya kuacha funguo za vyombo vyao vya usafiri. Habari hii kwa hisani ya MbeyaYetu.Blog

 

 

 

Lunyamila achoka, amcharukia Papic



Edibily Jonas Lunyamila.
Na Saleh Ally
WINGA nyota wa zamani wa Yanga, Edibily Jonas Lunyamila, ameonyesha kuchoshwa na mambo yanavyoendelea ndani ya klabu hiyo hasa maandalizi ya kuwavaa Zamalek ya Misri na kumtaka Kocha Mkuu, Kosta Papic abadili mwelekeo.
Yanga inatarajia kucheza mechi yake ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Februari 17 na 19 dhidi ya Zamalek.
Lunyamila amesema, Yanga wamekuwa wakitumia muda mwingi kwa malumbano huku Papic akionekana kuwa sehemu ya malumbano hayo kila kukicha.
“Sidhani kama ni wakati wa Yanga kulumbana kila siku, kocha (Papic) kila siku anazozana na viongozi. Mara hataki kambi ya Mwanza, mara anahusika na suala la kuwakataa wachezaji fulani.
“Haiwezi kuisaidia Yanga katika kipindi hiki, anatakiwa kufanya kazi zake za kiufundi na kuwajenga wachezaji kisaikolijia. Siku zote malumbano hujenga makundi na hiyo itakuwa ni sumu kwa Yanga,” alisema Lunyamila aliyewahi kuisaidia Yanga kucheza robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwaka 1998.
“Papic ni kocha mwenye uzoefu, atumie muda mwingi na wachezaji wake na ikiwezekana ahusike kuwaambia hali ilivyo ngumu na mwisho wajitolee halafu kama kuna makosa wanaweza kuyarekebisha hapo baadaye.”
Aidha, Lunyamila aliwataka viongozi wa Yanga nao kuangalia uwezekano wa kufanya mambo kitaalamu au kusikiliza ushauri kutoka kwenye benchi lao la ufundi ili kuepusha mabishano.
Pia akasisitiza suala la umakini na kujitolea kwa wachezaji kwa kuwa hata kama kuna ugumu, basi Zamalek inaweza kung’oka kama wakijipanga.
Zaidi kuhusiana na Lunyamila na maandalizi ya Yanga, soma uchambuzi ukurasa wa 12.

 

Simba: Tunauza mechi yetu ya Kiyovu

 


UONGOZI wa klabu ya Simba umesema upo katika mazungumzo na kampuni ya Clouds Media Group kwa ajili ya kuingia mkataba wa kuiuza mechi yao ya marudiano dhidi ya Kiyovu kutokana na kuuona mpango huo unafaa.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, amesema wameona ni vyema na wao wakafanya mpango huo kama walivyofanya watani wao Yanga.
“Mpango uliofanywa na Yanga wa kuikabidhi mechi yao ya Zamalek kwa Clouds Media Group ambayo imeidhamini na kuitangaza ni mzuri sana, hivyo na sisi tumeona ni bora tuingie katika mpango huo ili mechi yetu iweze kutangazika.
“Unajua mpira bila ya promosheni hauwezi kuwa mzuri, hivyo kwa upande wetu tumeliona hilo na tumeamua kulifanyia kazi na kwa sasa tunaendelea na mazungumzo na Clouds Media Group ili iweze kukubaliana nasi kudhamini kwa kuinunua mechi hiyo.
“Litakuwa ni jambo jema kwetu kwani mpango huo  utawawezesha watu wengi kuja kuiangalia mechi hiyo  kutokana na promosheni itakayofanyika,” alisema Kamwaga.
Aliongeza kuwa wapo katika mikakati madhubuti ya kuhakikisha wanajipanga ipasavyo ili waweze kufanya vizuri katika mchezo huo ambao utakuwa na ushindani wa hali ya juu kutokana na ubora wa timu hiyo.
“Tutaangalia uwezekano wa kucheza mechi moja ya kirafiki ya kimataifa katikati ya ligi na kama itashindikana, tutatumia mechi za ligi kuu kama maandalizi ya mchezo huo,” alisema Kamwaga.
Simba inatarajiwa kuvaana na Kiyovu ya Rwanda kati ya Februari 17 na 19 jijini Kigali katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika na kurudiana kati ya Machi mbili hadi nne jijini Dar es Salaam.

  0 comments

MAN U YAITUNGUA ARSENAL GOLI 2 KWA 1 NYUMBANI KWAO

Headmaster: Antonio Valencia heads Manchester United into a first-half injury time leadMchezeji wa Man United Valencia akionekana juu kwa juu akitingisha wavu kwa bao alilofunga kwa kichwa  katika dakika ya 45 kipindi cha kwanza, baada ya vuta ni kuvute ya mechi hiyo kati Manchester United Vs Arsenal
Dan's the man: Welbeck pounced from inside the box to restore Manchester United's lead
Mchezaji wa Man United Welbeck akifunga bao la pili.
 Katika dakika dakika 80 Welback alitingisha wavu tena kwa bao la pili na kusababisha Man United kutoka kidedea kwa bao 2-1 dhidi ya Arsenal.
Mpira uliendelea kwa kasi, vuta ni kuvute timu zote mbili zilikuwa zikifanya mashambulizi ya kushinda mchezo huo kwa matumaini ya kutuliza mpira chini, kwa utulivu na  makini, kipindi cha pili dakika 71 mchezaji wa Arsenal Robin van Persie kusawazisha bao 1-1 katika mchezo huo uliochezwa leo hii.

Kizaa zaa kiliaza tena pale timu ya Man United  kubadilisha mchezo baada ya timu Arsenal  kusawazisha bao hilo.


Mzee Yusuf atoa burudani tosha kwa Watanzania wanaoishi katika jiji la New York City

Mamia ya Watanzania wanaoishi jijini New York  jana jumamosi Jan 21,2012 wamiminika katika ukumbi wa The Portuguese American Club Moun Vernon, New York  kumuunga mkono na kumkaribisha rasmi, muimbaji marufu wa miondoko ya rusha roho,  maarufu kwa jina la Mzee Yusuf  ikiwa ni mara yake ya kwanza muimbaji huyo kuwasili na kutumbuiza jijini hapo. Picha kwa hisani ya VIJIMAMBO





No comments:

Post a Comment