Tuesday, January 8, 2013

ITSSSSSS MESSI AGAIN - AWAFUNIKA RONALDO NA INIESTA NA KUVUNJA REKODI YA KUCHUKUA BALLON D'OR KWA MARA 4 MFULULIZO



Lionel Messi - Kiboko asiyeshindika
Wapinzani
Kocha Bora wa Mwaka Vicente Del Bosque
Mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi ametwaa tuzo ya uchezaji bora wa dunia kwa mara ya nne mfululizo akiwafunika Cristiano Ronaldo na mchezaji mwenzie wa Barcelona Andres Iniesta katika sherehe za tuzo hizo zilizofanyika muda mfupi uliopita huko nchini Uswisi.

Timu bora ya Mwaka
Wakati huo huo ligi kuu ya Spain La liga imetoa wachezaji wote wanaounda kikosi cha FIFA cha mwaka 2012. Barcelona na Real Madrid wakitoa wachezaji watano kila timu moja, huku Atletico Madrid wakitoa mchezaji mmoja.

Ronaldo na Messi wakivunja rekodi ya kuwemo kwenye kikosi hicho kwa mara 6 mfululizo. Casillas ameingia mara 5.

Wachezaji wanaounda timu hiyo ni -

Goalkeeper: Iker Casillas
Defenders: Dani Alves, Gerard Pique, Sergio Ramos, Marcelo
Midfielders: Xabi Alonso, Xavi Hernandez, Andres Iniesta
Forwards: Lionel Messi, Radomel Falcao, Cristiano Ronaldo

No comments:

Post a Comment