Friday, October 5, 2012

Wanafunzi wa shule za sekondari za Makongo, St Mary na Mama Salma Kikwete washuhudia sarakasi za Tigo Mama Africa


Wanafunzi wa shule za sekondari za Makongo, St Mary na Mama Salma Kikwete washuhudia sarakasi za Tigo Mama Africa

Mtaalamu wa Biashara na Masoko wa Tigo, Gaudence Mushi (kulia) akizungumza na baadhi ya wanafunzi waliohudhuria onyesho la sarakasi la Tigo Mama Afrika lililodhaminiwa na Tigo katika Viwanja vya New World Cinema, Mwenge, jijini Dar es Salaam . Kushoto ni mwalimu wa Shule ya Sekondari Makongo, John Ngowi. Wanafunzi zaidi ya 1000 kutoka shule za sekondari za Makongo, St Mary na Mama Salma Kikwete walihudhuria.

Ofisa Uhusiano wa Tigo, Alice Maro (kushoto) akishakana mikono na Mwalimu wa Shule ya Sekondari Makongo, Kapteni Mstaafu, Hamisi Mfaume kabla ya onyesho la sarakasi la Tigo Mama Afrika kuanza. Katikati ni Mtaalamu wa Biashara na Masoko wa Tigo, Gaudence Mushi.
Baadhi ya wanafunzi wa sekondari wakipewa viburudisho kabla ya onyesho la sarakasi la Tigo Mama Africa kuanza
Wasanii wa kikundi cha sarakasi cha Mama Afrika, wakitoa burudani katika onyesho la sarakasi la Tigo Mama Afrika
Wasanii wa kikundi cha sarakasi cha Mama Afrika, wakitoa burudani katika onyesho la sarakasi la Tigo Mama Afrika
Baadhi ya wanafunzi waliohudhuria onyesho la sarakasi la Tigo Mama Afrika wakishangilia wakati wasanii wa kikundi hicho wakionyesha umahiri wao katika onyesho lililodhaminiwa na Tigo katika Viwanja vya New World Cinema, Mwenge, Dar es Salaam jana. Zaidi ya wanafunzi 1000 kutoka shule za sekondari za Makongo, St Mary na Mama Salma Kikwete walihudhuria.(PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE)

No comments:

Post a Comment