Thursday, June 28, 2012





Hali Mbaya: Hospitali ya Mkoa Mbeya yazidiwa na wagonjwa wanaokimbilia hospitalini hapo kupata huduma ya matibabu hasa waja wazito


Hii ndio Hali hali halisi katika Hospitali ya Mkoa Mbeya, huku wakina mama wajawazito wakiwa wamelala wawili mpaka wa tatu katika Kitanda kimoja.

Wakina mama hao ambao wengi wao wamekimbia katika Hospitali ya Wazazi Meta baada ya kukosa huduma ya matibabu ya uzazi kutokana na mgomo wa Madactari unao endelea Nchi nzima

Baadhi ya kina mama wajawazito wakiwa katika foleni ya kungoja kumuona Dactari

Mama Sophia Mwangwata kutoka Tunduma akiwa amemleta mwanae kuja kujifungua katika hospitali ya mkoa Mbeya , baada ya kukosa huduma huko Tunduma.

Wakina mama walio jifungua salama wamemshukuru sana mganga wa hospitali hiyo ,kwa huduma waliyo pata kujufungua salama, huku wengine wakisema Madactari walio goma hawana wazazi wala watoto wanao umwa

Hiki ndicho chumba kikuu cha upasuaji, Madactari walio kuwepo eneo hilo wamegoma kutokeza kwenye Kamera ya Mbeya yetu lakini wamedai kuwa , kila siku zaidi ya wanawake 15 hujifungua kwa njia ya upasuaji,hivyo kufanya kazi hiyo ya upasuaji kuwa ngumu sana na kuwaomba madactari wenzao warejee kazini ili waweze kusaidiana kazi hiyo,kwani wagonjwa ni tofauti na Chuma au Gari hawana Spea, Tofauti na magari unaweza ngoja spea ndio ukarekebisha lakini kwa Binadamu ukingoja atakufa.

Mama akiwa amelala Chini ya Godoro pamoja na kachanga kaliko zaliwa muda si mrefu uliopita

Umati wa wagonjwa unazidi kuongezeka katika Hospitali hiyo ya mkoa Mbeya

Hili Ndilo jengo la Hospitali ya Mkoa Mbeya
Picha zote na Blog ya Mbeya yetu

No comments:

Post a Comment