Tuesday, April 10, 2012

 

 

 

 

 

 

TASWIRA ZA NDEGE YA ATC ILIYOPATA AJALI KIGOMA LEO

Ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATC), aina ya Dash 8-300 iliyokuwa inatoka Kigoma kwenda Dar es Salaam kupitia Tabora, ikiwa imeanguka jana baada ya kuteleza kutokana na tope jingi kuwepo kwenye njia ya kurukia ya Uwanja wa Ndege wa Kigoma. Abiria 35 na wafanyakazi wanne walinusurika kwenye ajali hiyo
Wananchi wakiangalia ajali ya ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATC), aina ya Dash 8-300 iliyokuwa inatoka Kigoma kwenda Dar es Salaam kupitia Tabora, ikiwa imeanguka jana baada ya kuteleza kutokana na tope jingi kuwepo kwenye njia ya kurukia ya Uwanja wa Ndege wa Kigoma. Abiria 35 na wafanyakazi wanne walinusurika kwenye ajali hiyo.
 Hali ya ndege inavyoonekana upande wa kushoto.
 Hali ilivyokuwa inaonekana ndani ya ndege baada ya ajali kutokea jana katika Uwanja wa Ndege wa Kigoma.Picha kwa hisani ya Full Shangwe Blogu

 

 

Uzinduzi wa Miss Tabata 2012 wafana vilivyo

 Warembo wa wanaoshiriki shindano la kumsakama Malkia wa Tabata 2012 wakipozi mbele ya mashabiki wa burudani ya urembo jijini Dar es Salaam waliohudhuria uzinduzi wa shindano hilo la Urembo katika Ukumbi wa Dar West Park Tabata jana. Picha Zote na Father Kidevu Blog
 Warembo wakicheza Show maalum ya utambulisho wao. Goma la Don’t Take My Number ndo liliwaongoza.
Warembo wa wanaoshiriki shindano la kumsakama Malkia wa Tabata 2012 wakipozi mbele ya mashabiki wa burudani ya urembo jijini Dar es Salaam waliohudhuria uzinduzi wa shindano hilo la Urembo katika Ukumbi wa Dar West Park Tabata jana.
 Washiriki wa Shindano la Miss Ukonga 2012 ndio waliowasindikiza majirani zao wa Tabata.
 Mpiga drams wa Twanga Pepeta Martin Kibosho akifanya vitu vyake jukwaani.
 Mwimbaji mkongwe asiyechoka wala kuzeeka, Mumin Mwijuma akikamua na kundi lake la Twanga Pepeta.
 Wanenguaji wa Bendi ya Twanga Pepeta wakishambulia Jukwaa vilivyo. 
 Jopo la waandaaaji wa Shindano la Miss Chan'gombe walikuwepo kuangalia vitisho vya Miss Tabata 2011. Kushoto ni Mmoja wa washiriki wa Miss Chang'ombe ambaye hakika ni fimbo ya ukweli.
 Mwana dada Aisha Ramadhani "Aisha Mashauzi" aliwashika vilivyo na walikatika nyonga ile mbaya kwa taarabu yake kali.
Wadau mbalimbali wa Burudani na Urembo walihudhuria katika uzinduzi huo ulioenda sambamba na Show kali kutoka kwao Twanga Pepeta “Kisima cha Burudani” na Mashauzi Clasic Modern Taarab kutoka kwake Mtoto wa Kikurya Aisha Ramadhani  ‘Mashauzi’. Picha na Father Kidevu Blog

No comments:

Post a Comment