Thursday, October 4, 2012

AJALI MBAYA IMETOKEA ENEO LA MBALIZI MBEYA, MAGARI MAWILI YAGONGANA NA KUWAKA MOTO . WATU KUMI WALIPOTIWA KUFARIKI DUNIA, MBUNGE WA VITI MAALUM MH.MARY MWANJELWA ALIKUWEMO KATIKA AJALI HIYO, KATIBU WAKE ATEKETEA KWA MOTO

Tuesday, October 2, 2012


AJALI MBAYA IMETOKEA ENEO LA MBALIZI MBEYA

AJALI MBAYA IMETOKEA ENEO LA MBALIZI MBEYA, MAGARI MAWILI YAGONGANA NA KUWAKA MOTO . WATU KUMI WALIPOTIWA KUFARIKI DUNIA, MBUNGE WA VITI MAALUM MH.MARY MWANJELWA ALIKUWEMO KATIKA AJALI HIYO, KATIBU WAKE ATEKETEA KWA MOTO. 

WATU 10 wamakufa papo hapo ajalini, 20 wakijeruhiwa akiwemo Mbunge Mary Mwanjelwa‏,kibaka nae kwenye mishe eneo la tukio aambulia mauti dunia imekwisha !!


 HIVI NDIVYO HILI GARI LILIVYO UNGUA MOTO BAADA YA AJALI

HILI NDILO GARI ALILOKUWEMO MBUNGE MARY MWANJELWA LIMETEKETEA LOTE KWA MOTO


 HIVI NDIVYO HILI GARI LILIVYO UNGUA MOTO BAADA YA AJALI
 MAMIA YA WATU WALIOFIKA KUSHUHUDIA AJALI HIYO MBALIZI
HAYA NI MABAKI YA GARI HILI AMBALO NALO LILIUNGUA LOTE


 HIVI NDIVYO GARI HILI LILIVYO PINDUKA NA KUWAKA MOTO BAADA YA AJALI
 HII NI GARI NYENGINE AMBAYO PIA ILIWAKA MOTO BAADA YA KUGONGANA 
 FIRE WAKIWA WAMEWAHI ENEO LA TUKIO KWA AJILI YA KUZIMA MOTO HUO
Mkuu wa mkoa Mbeya Abas Kandoro akiangalia ajali liyotokea mbalizi mbeya mchana wa leo
 MKUU WA MKOA WA MBEYA ALIYE VAA SUTI YA BLUE MH. ABASS KANDORO AKIWA ENEO LA AJALI

Watu zaidi ya kumi wamekufa baada ya lori la mafuta kufeli breki na kuyagonga magari mengine matatu katika mtelemko wa mlima wa Iwambi – Mbalizi nje kidogo ya Jiji la Mbeya.
WANANCHI MBALI MBALI WAKIWA WANASHUHUDIA AJALI HUKU WENGINE WAKIWA WANAENDELEA KUOKOA WALIO PATA AJALI

Baadhi ya watu waliioshuhudia ajali hiyo, walisema kuwa lori hilo la mafuta lilifeli breki na kuanza kutelemka kwa kasi katika mlima huo, ambapo liliyagonga magari matatu ukiwamo Hiace yenye namba za usajili T 587 AHT.

Kwa upande wake, Muuguzi wa Hospitali ya Ifisi, Sikitu Mbilinyi  alisema mbunge Mwanjelwa analalamika zaidi maumivu katika sehemu ya mgongoni  na miguu  sawa na dereva wake ambaye naye analalamikia miguu na amepasuka sehemu ya kichwani.

KIKOSI CHA FFU NAO WALIKUWEPO SAMBAMBA KATIKA KUHAKIKISHA ZOEZI LA UOKOAJI LINAENDA KIKAMILIFU.
PIA KATIKA ENEO HILI  MBUNGE WA VITI MAALUM MH.MARY
MWANJELWAALIKUWEPO NDANI YA PICK UP ILIYO UNGUWA MOTO, KATIBU WAKE ATEKETEA KWA MOTO  
 
wakati huo wananchi wakiwa katika uokoaji si ndo akatokea kibaka ama kweli UKISTAAJABU ya Musa utayaona ya firauni huo ndo msemo pekee ambao naweza kuutumia katika kukujuza yaliyotokea mapema mchana wa leo katika ajali mbaya eneo la mbalizi Mbeya vijijini
em shuhudia mwenyewe ujionanee yalomkuta kibaka uyooo







Wakati wengine wakiendelea kuokoa majeruhi wengine wamejikuta wakifanya tofauti na vile ilivyotegemewa pale kijana mmoja alipojitoa mhanga na kuingia katika mmojawapo wa waokoaji na kutaka kumchomolea fedha “ waswahili huita mshiko”.
Asalale kijana huyo ambaye hajafahamika jina mpaka mauti yanamkuta katika tukio hilo alikwidwa na mashuhuda wa ajali hiyo na kupewa kichapo cha mbwa mwizi wa kuku.

No comments:

Post a Comment